Ihefu: Tunakuja Kivingine Msimu Ujao

WAKATI wakijiandaa na msimu ujao, Uongozi wa klabu ya Ihefu umetamba kuja kivingine wa Ligi Kuu Bara.

Ihefu inatarajia kushiriki ligi kuu kwa msimu ujao baada ya kupanda daraja wakiwa mabingwa wa michuano ya Championship.

Akizungumzia hali ya kambi yao, Ofisa Habari wa Ihefu, Peter Andrew amesema kuwa “Kikosi kinaendelea na maandalizi ya msimu ujao na kila kitu kipo sawa.

“Wachezaji wanaonekana kuwa na morali kubwa ya kusubiri ligi na tunatarajia kucheza mechi ya kirafiki ya mashindano ya Mbeya Super Cup na hizo tutatumia kwa ajili ya pre season ‘maandalizi’.

“Timu itakuwa vizuri sana kwa msimu ujao na tunaahidi kuja kivingine kwani tumefanya usajili mzuri.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.