ASUBUHI ya leo, kumeibuka taarifa juu ya mshambuliaji wa Simba Kibu Denis kutakiwa na klabu ya Yanga.
Taarifa zinadai kuwa, Yanga wamemuandalia mkataba wa miaka mitatu wenye thamani ya milioni 300 na atakua akikunja milioni 12 kwa mwezi.
Huku ikielezwa kuwa Simba wameshtuka na wanapambana kumbakiza Mchezaji huyo klabuni hapo, lakini Kibu Denis bado hajafanya maamuzi yoyote hadi Sasa.
Meridian Sports ilimtafuta mmoja wa viongozi wa Yanga Ili kujua undani wa taarifa hizo, naye alisema ni kweli mchongo huo upo na Yanga wanamtaka, huku akiomba hifadhi ya jina lake.


