Kocha Msauz Atua Simba

BAADA ya kelele nyingi kutoka kwa mashabiki na wachambuzi nchini, hatimaye klabu ya Simba imetambulisha rasmi kocha wa viungo Kelvin Mandla raia wa Afrika Kusini.

Mandla, anajiunga na benchi la ufundi linaloongozwa na Kaimu Kocha Mkuu Juma Ramadhan Mgunda na atapishana na kocha msaidizi Seleman Matola (Veron).

Simba haikuwa na kocha wa viungo baada ya kuondoka Sbai Karim aliyeongozana na aliyekua Kocha wa Klabu hiyo kutoka Serbia Zoran Maki aliyeondoka ndani ya Simba baada ya kukaa kwa muda mfupi sana.

Kocha Mandla alitangazwa kupitia Simba App na kurasa za mitandao za klabu hiyo jana Alhamis. Huyo anakua kocha wa pili kutambulishwa ndani ya klabu hiyo baada ya kutambulishwa Chlouha Zakaria, ambaye ni kocha wa makipa.

Mandla atakuwa kwenye benchi la ufundi kwa mara ya kwanza kesho Jumamosi wakati Simba watakapovaana na Ruvu Shootinga kwenye uwanja wa Mkapa.


Kombe la Dunia Linatimua Vumbi huko Qatar ni timu 32, sawa na mechi 64 zitapigwa kwenye viwanja tofauti. Meridianbet wana uwanja wao wa Kushiriki na wewe wakati Michuano hii inaendelea.

Uwanja wa Machaguo Spesho ni Kwa ajili yako, wewe Bingwa wa Kubeti. Unaweza kubeti ni Timu gani itachukua Ubingwa, Timu gani Itaongoza kuwa na kadi nyingi za Njano na Nyekundu, au Timu gani itatoka mapema kwenye michuano hiyo. Uamuzi ni wako. Chaguo ni lako. Hii ipo mpaka mwisho wa Kombe la Dunia.

BONYEZA HAPA

Makala iliyopita

Acha ujumbe