Mastaa Simba Watoa Ahadi Hii, Walivyokutana na MO Dewji.

“NYIE TULIENI TU” ni kauli ya Mastaa wa Simba walivyotoa ahadi mbele ya kikao kizito kilichoitishwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi na Rais wa Heshima wa Simba, Mohammed ‘Mo Dewji’ kabla ya jioni ya leo Julai 8 kuanza sfari ya kwenda Ismailia, Misri kujiandaa na msimu mpya wa mashindano 2024/25. Jisajili hapa kuwa wa kwanza kushinda Mamilioni ya Meridianbet kila siku.

Klabu ya Simba inaondoka kwenda Misri kuanza safari mpya ya kimageuzi chini ya Bilionea, Mo Dewji aliyerudi na jeuri akisajili kikosi kizito na kushusha benchi la ufundi kutoka Afrika Kusini chini ya Fadlu Davids ambalo nalo pamoja na wachezaji walifanya kikao kizito na Bodi ya Wakurugenzi kuwekana sawa.

 

Mastaa wa Simba
Kiungo Mchezeshaji wa Simba SC Deborah Fernandes akishikana mikono na Mohamed Dewji, kwenye kikao cha pamoja na wachezaji wote wa Simba na Viongozi wa klabu hiyo.

Hadi sasa Simba inajumla ya wachezaji wa Kimataifa 16 huku baadhi yao wakitarajiwa kupewa Thank You muda wowote, ina Ayoub Lakred, Valentin Nouma, Che Malone Fondoh, Chamou Karaboue, Augustine Okejepha, Fabrice Ngoma, Sadio Kanoute, Babacar Sarr, Deborah Farnandes, Joshua Mutake, Willy Essomba Onana, Par Omar Jobe, Fred Michael Koublan, Steve Mukwala, Jean Charles Ahoua, Aubin Kramo.

Hata hivyo baadhi ya wachezaji waliopewa mkono wa kwaheri klabuni hapo ni John Bocco, Saidoo Ntibazonkiza, Kennedy Juma, Luis Miquissone, Clatous Chama, Henock Inonga Baka aliyeuzwa AS FAR RABAT ya Morocco.

Jiandae kubeti na Meridianbet kwa ushindi mkubwa na odds kubwa, Ligi  zinakaribia kuanza,  usije kupishana na gari la Mshahara.

Endapo Simba itaachana Sadio Kanoute, Babacar Sar, Jobe, Onana na Aubin Kramo Simba itabakiza nafasi moja kukamilisha idada ya wachezaji 12 wa Kimataifa, nafasi hiyo anayopewa zaidi ni Elie Mpanzu wa AS Vita ambaye usajili wake upo karibuni kukamilika.

Simba itaondoka kwenda Misri kwaajili ya kuweka kambi ya wiki 2 kabla ya kurudi nchini kujiandaa na Tamasha kubwa la Simba Day, ambalo limepangwa kufanyika Agosti 3, huku pia wiki inayofuatia Simba watakabiliwa na mchezo mgumu wa Ngao ya Jamii dhidi ya mahasimu wao wa Karaikoo, Yanga mechi hiyo itapigwa Agosti 8.

Kasino ya Mtandaoni usipange kuacha kucheza, Meridianbet wameakuandalia Maokoto na bonasi za kasino kibao.

Acha ujumbe