Mtibwa Sugar Waahidi Kufanya Makubwa Msimu Huu

BAADA ya ratiba ya ligi kuu kutangazwa rasmi leo, Uongozi wa Mtibwa Sugar umetamba kuwa hawauogopi mchezo wao wa kwanza dhidi ya Namungo na watafanya makubwa kwa msimu ujao.

Mchezo huo wa ligi kuu Bara kwa msimu wa 2022/23 unatarajiwa kupigwa Agosti 15 mwaka huu kwenye Uwanja wa Majaliwa, Lindi.

Akizungumzia hilo Ofisa Habari wa Mtibwa Sugar, Thobias Kifaru amesema kwamba “Hatuna shaka na ratiba iliyopangwa kwani tumejiandaa vizuri kwa ajili ya kuhakikisha tunafanya vizuri.

“Tumeachana na nyota 19 ambao tulikuwa nao msimu uliopita waliopelekea kucheza playoffs kwa misimu iliyopita hivyo kwa sasa tuna jeshi kubwa la maangamizi.

“Tunatarajia kuonyesha ushindani mkubwa kwa msimu ujao hivyo niwatoe wasiwasi mashabiki wetu kwamba Mtibwa itakuwa ya moto sana msimu ujao na tuko vizuri sana, tutafanya makubwa msimu huu.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.