Nyota Pan Kuanza Tizi Kesho

WACHEZAJI wa Pan African inayoshiriki michuano ya Championship, wanatarajia kuanza mazoezi kesho jumanne kwa ajili ya kujiandaa na mchezo dhidi ya Mbuni.

Mchezo huo unatarajiwa kupigwa Oktoba 2, mwaka huu ambapo kikosi hicho tayari kimecheza mechi mbili na kukusanya pointi moja.

 

Pan

Akizungumzia hilo, Ofisa Habari wa Pan African, Leen Essau amesema kuwa “Baada ya michezo yetu miwili dhidi ya Kitayosce na Mashujaa, timu imerejea Dar tayari.

“Mazoezi yataanza rasmi kesho kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wetu wa ligi unaofuata dhidi ya Mbuni ambao tutacheza kwenye Uwanja wa Uhuru.

 

PAN

 

Acha ujumbe