Pan Waanza Kutamba Championship

Baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Fountain Gate kikosi cha Pan African kitarejea mazoezini kesho kujiandaa na mchezo ujao wa Championship.

Pan itashuka tena dimbani Novemba 19 mwaka huu kumenyana na Copco ya Jijini Mwanza kwenye Uwanja wa Nyamagana.

Akizungumza hali ya kikosi chao, Ofisa Habari wa Pan African, Leen Essau amesema: “Kikosi chetu kitarejea mazoezini kesho jumanne kujiandaa na mchezo mwingine wa ligi dhidi ya Copco.

“Tuna furaha sana baada ya kupata ushindi wa jana hivyo kuelekea kwenye mchezo huo dhidi ya Copco basi wajiandae na kipigo.

“Mipango yetu inaendelea vizuri na ushindi huu unaongeza morali kwa wachezaji, benchi la ufundi katika kutimiza malengo yetu msimu huu.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.