Mwamba Fadlu Davids Kocha Mkuu wa Simba ana kibarua cha kusuka upya kikosi hicho kuelekea msimu wa 2024/25 ambao unatarajiwa kuwa na ushindani kitaifa na kimataifa.
Simba kwenye Kombe la Shirikisho Afrika itasubiri mshindi wa mchezo kati ya Uhamiaji dhidi ya Libya kwa kuwa haitaanzia hatua ya awali.
Mbali na Msimbazi kupeperusha bendera ya Tanzania kwenye Kombe la Shirikisho, Coastal Union pia ipo anga la kimataifa baada ya kugotea nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi.
Ahmed Ally, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Mnyama amesema: “Kocha Fadlu anatambua kitu ambacho Wanamsimbazi wanahitaji hivyo anasuka kikosi kazi kwa ajili ya kuleta ushindani akishirikiana na benchi zima la ufundi.”
Wachezaji wapo tayari wanaendelea na mazoezi na wapo wachezaji wapya na wale waliokuwa na kikosi kwa msimu wa 2023/24 tunaamini kwamba tutafanya vizuri mashabiki wazidi kuwa pamoja nasi.
This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.
Strictly Necessary Cookies
Strictly Necessary Cookie should be enabled at all times so that we can save your preferences for cookie settings.
If you disable this cookie, we will not be able to save your preferences. This means that every time you visit this website you will need to enable or disable cookies again.