SIMBA WAWATUMIA SALAMU DODOMA JIJI FC

Kesho Jumapili Simba watakuwa nyumbabi KMC Complex kuvaana na Simba kwenye mchezo mwingine muhimu kwao msimu huu kwenye harakati zao za kuwania ubingwa na wanakwenda kwenye mchezo huo wakiwa na kumbukumbu wawili hao ya kutoka sare kwenye mchezo wa kwanza.

SIMBA WAWATUMIA SALAMU DODOMA JIJI FC

Huku viongozi wa Simba wakitoa tahadhari kubwa kwa wapinzani wao hao, wakisema wao wanahitaji ushindi kwenye kila mchezo wanakwenda kwenye mchezo huo wakiwa na sura tofauti kabisa.

Huku wakisema wanaelewa Dodoma Jiji FC imekuwa ikitoa ushindani na matokeo yasiyotabirika inapokutana na timu kubwa. Wamewahi kuwatibua Yanga SC kwa matokeo ya kushangaza na pia kuwapa wakati mgumu Simba SC kwa sare katika michezo ya nyuma. Rekodi hiyo imewajengea sifa ya kuwa “timu hatari kwa vigogo”, jambo linaloongeza tahadhari kwa wapinzani wao.

Wekundu wa Msimbazi wanaingia katika mchezo huo wakiwa na presha ya kuendeleza ushindani mkali katika mbio za ubingwa wa ligi, huku wakijua kuwa makosa madogo yanaweza kuwagharimu pakubwa. Licha ya ubora na kina cha kikosi chao, bado wanatambua kuwa Dodoma Jiji mara nyingi hucheza kwa ujasiri mkubwa wanapokutana na timu kubwa.

Beki wa Mnyama, Nickson Kibabage, amesisitiza kuwa mchezo huo hautakuwa mwepesi kama watu wengi wanavyoweza kufikiria, akibainisha kuwa wapinzani wao wana nidhamu na mpangilio mzuri wa kiuchezaji.

SIMBA WAWATUMIA SALAMU DODOMA JIJI FC

“Haitakuwa mechi rahisi. Dodoma Jiji wana wachezaji wazuri na timu iliyopangika vizuri, hivyo tunapaswa kuwa makini kuanzia mwanzo hadi mwisho,” amesema Afisa Habari Ahmed Ally, akisisitiza umuhimu wa Simba kucheza kwa umakini wa hali ya juu.

Kauli hiyo imeongeza hamasa na presha kuelekea pambano hilo, huku mashabiki wakisubiri kuona kama Simba SC wataendelea kuthibitisha ubabe wao katika mbio za ubingwa au Dodoma Jiji FC wataendeleza historia yao ya kushtua vigogo wa ligi.

Kwa ujumla, macho na masikio ya wadau wa soka yatakuwa KMC Complex, ambapo pambano hilo linatarajiwa kutoa ushindani mkali na huenda likaweka wazi mwelekeo wa mbio za ubingwa mapema kabisa.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.