Singida Big Stars Hawataki Masihara

UONGOZI wa kikosi cha Singida Big Stars umefunguka kuwa hawataki masihala kwa msimu ujao kwani wanahitaji kumaliza katika nafasi tatu za juu kwenye msimamo wa ligi. 

Mtendaji Mkuu wa timu ya Singida Big Stars, Muhibu Kanu amefunguka kuwa mipango yao ni kumaliza kwenye nafasi tatu za juu kwenye msimamo wa ligi kwa msimu ujao.

“Hakuna kingine zaidi ya kumaliza katika nafasi tatu za juu ikiwezekana kubeba kabisa ubingwa, kwani sisi tunakuja katika ligi kushindana sio kushiriki.

“Na hilo limethibitika kutokana na usajili bora tuliofanya wa wachezaji wenye uzoefu na kiwango kikubwa cha kucheza soka.

“Wapinzani wajiandae vema, hatutaki kufanya masihara kabisa kwa msimu ujao ambao tunaamini utakuwa mgumu kutokana na ushindani uliokuwepo wa timu.”

 

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.