Kocha wa Coastal Union, Fikiri Elias, amesema kikosi chake kipo tayari kwa mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya TRA United utakaochezwa Juni 24, 2026, akieleza kuwa timu yake imejipanga kuonesha soka la kuvutia na kuondoka na matokeo chanya katika mchezo huo muhimu.
“Tumejiandaa kupeleka ushindani na kuonesha burudani ya soka. Maandalizi yamekamilika vizuri na wachezaji wamezoea hali ya hewa ya Arusha, jambo linalotupa matumaini ya kupata alama tatu,” alisema Fikiri wakati wa kuelezea maandalizi ya kikosi chake.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kwa upande wa wachezaji, Luician Kilua amesema morali ndani ya kikosi cha Coastal Union ipo juu huku kila mchezaji akiwa na hamu ya kupambana kwa nguvu zote ili kuhakikisha timu inapata ushindi muhimu katika hatua hizi za mwisho za msimu.
Naye Kocha wa TRA United, Etienne Ndayiragije, amesema kikosi chake kipo tayari kwa pambano hilo baada ya kukamilisha maandalizi yake, huku akifurahishwa na kurejea kwa baadhi ya wachezaji waliokuwa nje ya uwanja kutokana na majeraha. “Timu ipo katika hali nzuri na kurejea kwa wachezaji wetu waliokuwa majeruhi kumeongeza nguvu na chaguo ndani ya kikosi,” alisema Etienne.
Mchezaji wa TRA United, Ramadhan Salum ‘Chobwedo’, amesema timu hiyo inatarajia kutumia vyema faida ya kucheza nyumbani ili kupata ushindi utakaoweka hai matumaini yao ya kumaliza msimu katika nafasi nne za juu za msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.


