Uongozi wa klabu ya Yanga SC, umemuongeza mkataba wa miaka miwili beki wao wa kulia, Kibwana Shomari kuendelea kuitumikia klabu hiyo, mkatab huo utadumu hadi mwaka 2026.
Kibwana ambaye ameitumikia Yanga kwa miaka mitatu tangu ametua akitokea Mtibwa Sugar, ataendelea kubaki zaidi ndani ya timu hiyo ya Jangwani kwa miaka mingine miwili.
Beki huyo ambaye ametwaa mataji mawili ya Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho (FA) anaendelea kupambania nafasi mbele ya Kouassi Attohoula Yao ambaye amekuwa panga pangua katika kikosi cha kwanza tangu ametua akitokea ASEC Mimosas.
Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya Yanga kimefichua kuwa lilikuwa ni suala la muda kwa beki huyo kuongeza mkataba kutokana na uwezo aliouonyesha tangu ametua akitokea Mtibwa Sugar.
“Hatuwezi tukawa na beki mmoja wakati tuna mashindano mengi ya ndani na nje hivyo kuhusu kumuongeza mkataba Kibwana lilikuwa ni suala la muda tu sasa mambo yamekamilika,” kilisema chanzo hicho.
Hadi sasa, mastaa walioongezwa mikataba Yanga ni Djigui Diarra, Farid Mussa, Abuutwalib Mshery, Bakari Mwamnyeto, Jonas Mkude na Salum Abubakar ‘Sure Boy’.
Huku klabu hiyo ikiwa imewatambulisha kundini wachezaji wanne hadi sasa, Kiungo Clatous Chama aliyetoka Simba, Prince Dube mshambuliaji alikuwa ni mchezaji huru akitokea Azam FC, Chadrack Boka kutoka FC Lupopo ya DR Congo ni beki wa kushoto, halafu kuna Mlinda mlango wa Ihefu Abubakar Khomeiny.
This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.
Strictly Necessary Cookies
Strictly Necessary Cookie should be enabled at all times so that we can save your preferences for cookie settings.
If you disable this cookie, we will not be able to save your preferences. This means that every time you visit this website you will need to enable or disable cookies again.