Alex Korio Akutana na Rungu la AIU!

Mwanariadha kutoka Nairobi, Kenya amekutana na rungu kali la bodi inayosimamia michezo yao kwa kufanya kosa la kinidhamu. Mkenya huyo amesimamishwa kushiriki michezo kwa kupewa adhabu na Atheltics Integrity Unit (AIU) baada ya kushindwa kueleza ni wapi alikuwa wakati akitafutwa, tayari anaitumikia adhabu hiyo.

Hii inakuja ikiwa ni mwezi mmoja tu tangu bingwa wa 2017 London Marathon, Daniel Wanjiru kupigwa rungu kama hilo na bodi hiyo hiyo ya AIU.

Korio, ambaye ni bingwa wa 2017 Bengaluru 10 kilometa, pia, alikuwa ni sehemu ya waliochuana vikali na Eliud Kipchoge katika shindano la Ineos 1:59 nchini Vienna mwaka jana na mbio zake za mwisho kushiriki ni zile za umbali wa 10 kilometa zilizofanyika Valencia.

Mwanariadha kutoka Nairobi, Kenya amekutana na rungu kali la bodi inayosimamia michezo yao kwa kufanya kosa la kinidhamu. Mkenya huyo amesimamishwa kushiriki michezo kwa kupewa adhabu na Atheltics Integrity Unit (AIU) baada ya kushindwa kueleza ni wapi alikuwa wakati akitafutwa, tayari anaitumikia adhabu hiyo.

Mwanariadha huyu aliwakilisha taifa lake la Kenya kwenye 2019 World Athletics Championship ambapo alikuwa ni mshindi wa nafasi ya 11 kwenye mbio za umbali wa mita 10,000. Kwenye ubingwa wa kitaifa hivi karibuni alishika namba nne kiujumla.

Kwa adhabu hii sasa Korio anakuwa ni Mkenya wa sita kukutana na rungu la AIU baada ya Wanjiru, mwanamarathoni wa zamani aliyevunja rekodi ya kidunia Wilson Kipsang, Alfred Kipketer, Kenneth Kiprop na Mikel Kiprotich Mutai ambapo huyo wa mwisho alipizuiwa kwa kuwa na Madawa Yasiyoruhusiwa Michezoni (Norandrosterone).

23 Komentara

    Duh! Pole yake

    Jibu

    Sio kosa kubwa la kumpatia adhabu hiyo ikichukulia huyu n mwanariadhara bora dunian kwa kosa dogo kama hilo

    Jibu

    Kajiharibia sifa. Pole yake

    Jibu

    pole sana wa kenya ila udanganganyifu kwenye michezo cyo vzr

    Jibu

    Pole kijana..!azabu itaisha mambo mengine yataendelea..!

    Jibu

    Lazma Sheria zifuatwe ili iwe funzo kwa wengine…

    Jibu

    sheria lazima ifatwe..baadhi ya wana-riadha wababaifu

    Jibu

    Pole yake.atajifunza kutokana na makosa

    Jibu

    Mnatujuza mambo mengi ambayo hata atuyajue asanten kwa hilo

    Jibu

    Inaonekana wanatumia mazoea sana kuliko nidhamu ys mchezo

    Jibu

    Hatua za kinidham lazma zichukuliwe

    Jibu

    Lazma Sheria zifuatwe ili iwe funzo kwa wengine…

    Jibu

    Udanyanyifu sio mzuri pole yake

    Jibu

    Natumaini atajifunza atorudia tena

    Jibu

    Jamaa kajiharibia Sana kutumia madawa yaliyokatazwa michezoni

    Jibu

    Iyo safi sana na iwe funzo kwa wote wenye tabia kama zake

    Jibu

    Kajiharibia kazi na hiyo iwe fundisho kwa wengine

    Jibu

    lazima apeww adhabu

    Jibu

    Wamemuonea tu.

    Jibu

    safi sn cku nyngn atajifunza

    Jibu

    duuuh

    Jibu

    Duuuh

    Jibu

    Pole yake amejifunnza kutokana na makosa

    Jibu

Acha ujumbe