Ambokile Atua Nkana FC.


 

Mshambuliaji wa zamani wa Mbeya City, Eliud Ambokile amejiunga na Miamba ya Soka mjini Kitwe, Nkana FC ya Zambia Baada ya Wakati mgumu ndani ya klabu ya TP Mazembe ya DR Congo.

Ambokile alijiunga na TP Mazembe Mnamo Juni 2019 Baada ya kuwa na Kiwango Bora ndani ya Mbeya City ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

 

Ambokile (wa pili kulia) akiwa na wachezaji wenzie katika klabu yake ya zamani ya TP Mazembe.

Tangu Wakati huo amekuwa na wakati finyu wa kucheza na kwa muda sasa amekuwa akifanya mazoezi na Nkana Kabla ya kusaini Mkataba huu hii leo..

Nkana jana ili dimba la nyumbani, Nkana Stadium kuwaalika Green Buffaloes Katika Muendelezo wa Ligi Kuu Nchini Zambia ambapo walitoka sare ya 2-2.

Nkana ipo Nafasi ya 16 (tatu Kutoka mkiani) Baada ya Mechi 18 huku timu nyingine zikiwa zimecheza Mechi 20 na 21, Zesco United ndio vinara kwa alama 40.


UNAWEZAJE KUKOSA KASINO YA BREAK AWAY LUCKY WILDS INAYOKUPA NAFASI YA USHINDI MURUA.

Break Away Lucky Wilds ni moja ya Sloti pendwa katika kasino za #meridianbet inayokupa mara 11,000X ya dau lako, unayo nafasi ya kuwa milionea unasubiri nini?

CHEZA HAPA

3 Komentara

    Ambokile anajitahidi sana ila kabadilisha upepo

    Jibu

    Vizuri Sana

    Jibu

    Kila lakheri kwake eliud

    Jibu

Acha ujumbe