Vyanzo mbalimbali vinadai kuwa Andoni Iraola anatarajiwa kuichagua Crystal Palace badala ya AC Milan, jambo linalomaanisha kuwa chaguo zilizobaki kwa Rossoneri ni Xavi Hernández, Oliver Glasner na Mauricio Pochettino, huku Pochettino akiwa tayari ameshafanya mazungumzo na miamba hiyo ya Serie A.

Kocha wa zamani wa AFC Bournemouth, Iraola, anaonekana kuwa karibu zaidi kuichagua Crystal Palace kuliko Milan, kwa mujibu wa vyanzo kadhaa ikiwemo gazeti la La Gazzetta dello Sport na Sportmediaset.
Andoni Iraola aliibuka kama chaguo kuu la AC Milan kuchukua nafasi ya Massimiliano Allegri, lakini kocha huyo Mhispania anaonekana kuwa tayari zaidi kuichagua Crystal Palace kutokana na sababu za kifamilia na kitaaluma.
Kwa mujibu wa La Gazzetta dello Sport, Iraola yuko tayari kuendelea kubaki kwenye Premier League pia kwa sababu Milan ipo katika kipindi cha kujijenga upya, baada ya kuwafukuza viongozi wao wote pamoja na Allegri kufuatia kushindwa kufuzu kucheza UEFA Champions League.
Kwa kuwa Andoni Iraola anaelekea kujiunga na Crystal Palace, basi Oliver Glasner anaweza kuwa chaguo kwa AC Milan, kwa mujibu wa taarifa mbalimbali, sambamba na kocha wa zamani wa Barcelona, Xavi Hernández.



