Antonio Conte Amemtetea Højlund huku Man United Ikiendelea Kusubiri Uhamisho wa Kudumu.

Kocha wa Napoli, Antonio Conte, amesisitiza kuwa Rasmus Højlund bado ana nafasi kubwa ya kuimarika huku Partenopei ikiendelea kupambana kuhakikisha nafasi ya kucheza UEFA Champions League, jambo ambalo litafanya uhamisho wa kudumu wa Mdenmark huyo kutoka Manchester United kuthibitishwa moja kwa moja.

Antonio Conte Amemtetea Højlund huku Man United Ikiendelea Kusubiri Uhamisho wa Kudumu.

Napoli ilipata kipigo cha mabao 3-2 nyumbani dhidi ya Bologna Jumatatu, na kushindwa kuthibitisha rasmi kufuzu kwa UEFA Champions League ikiwa bado zimebaki mechi mbili.

Rasmus Højlund alianza mchezo huo lakini hakufanikiwa kufunga, hata hivyo kocha wa Partenopei, Antonio Conte, alimtetea mshambuliaji huyo anayekipiga kwa mkopo kutoka Manchester United.
“Tusisahau kwamba yeye ndiye mshambuliaji pekee tuliyenaye kwenye kikosi kwa sasa, hivyo anacheza karibu kila wakati,” alisema Antonio Conte baada ya mchezo kumalizika.

“Ningependa kuwa na nafasi ya kumpumzisha kidogo. Ni kijana, ana nguvu nyingi, na kuna nyakati unatakiwa kushambulia nafasi, nyingine unatakiwa kushikilia mpira. Ana miaka 23 tu, anafanya kazi kubwa kwa ajili ya timu na bado ana nafasi ya kuendelea kuimarika.”

Rasmus Højlund amefunga mabao 14 katika mechi 42 kwenye mashindano yote msimu huu.

Antonio Conte Amemtetea Højlund huku Man United Ikiendelea Kusubiri Uhamisho wa Kudumu.

Mdenmark huyo yupo Napoli kwa mkopo kutoka Manchester United, lakini Napoli ina chaguo la kufanya uhamisho wake kuwa wa kudumu kwa euro milioni 44.

Chaguo la Napoli kumchukua moja kwa moja Rasmus Højlund litakuwa la lazima iwapo watatinga UEFA Champions League, lakini kwa sasa bado hawajathibitisha kumaliza ndani ya nafasi nne za juu huku zikiwa zimebaki mechi mbili pekee.

Mkurugenzi wa Napoli, Giovanni Manna, mara kadhaa amesema kuwa klabu hiyo itafanya uhamisho wa Hojlund kuwa wa kudumu majira ya kiangazi bila kujali kama watatinga UEFA Champions League au la.

Napoli bado ipo kwenye nafasi nzuri ya kufuzu UEFA Champions League, ikiwa nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi kwa tofauti ya pointi tatu dhidi ya AS Roma na AC Milan, ambazo zinalingana kwa pointi 67 katika nafasi ya nne.

Wikiendi ijayo, Partenopei watasafiri kucheza dhidi ya Pisa ambao tayari wameshuka daraja, kabla ya kumaliza kampeni yao nyumbani dhidi ya Udinese wikiendi ya Mei 24.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.