Kocha wa Napoli, Antonio Conte, amesisitiza kuwa Rasmus Højlund bado ana nafasi kubwa ya kuimarika huku Partenopei ikiendelea kupambana kuhakikisha nafasi ya kucheza UEFA Champions League, jambo ambalo litafanya uhamisho wa kudumu wa Mdenmark huyo kutoka Manchester United kuthibitishwa moja kwa moja.

Napoli ilipata kipigo cha mabao 3-2 nyumbani dhidi ya Bologna Jumatatu, na kushindwa kuthibitisha rasmi kufuzu kwa UEFA Champions League ikiwa bado zimebaki mechi mbili.
Rasmus Højlund alianza mchezo huo lakini hakufanikiwa kufunga, hata hivyo kocha wa Partenopei, Antonio Conte, alimtetea mshambuliaji huyo anayekipiga kwa mkopo kutoka Manchester United.
“Tusisahau kwamba yeye ndiye mshambuliaji pekee tuliyenaye kwenye kikosi kwa sasa, hivyo anacheza karibu kila wakati,” alisema Antonio Conte baada ya mchezo kumalizika.
“Ningependa kuwa na nafasi ya kumpumzisha kidogo. Ni kijana, ana nguvu nyingi, na kuna nyakati unatakiwa kushambulia nafasi, nyingine unatakiwa kushikilia mpira. Ana miaka 23 tu, anafanya kazi kubwa kwa ajili ya timu na bado ana nafasi ya kuendelea kuimarika.”
Rasmus Højlund amefunga mabao 14 katika mechi 42 kwenye mashindano yote msimu huu.



