Aliyewahi kuwa mchezaji na nahodha wa Man United, Antonio Valencia, ameamua kutundika daluga na kuachana na mchezo wa soka kama mchezaji.
Valencia alisajiliwa na United akitokea Wigan Athletic (2009). Alifanikiwa kubeba mataji mawili ya EPL, Kombe 1 la FA Cup, makombe mawili ya Kombe la Ligi, Ngao 3 za hisani na kombe 1 la Europa wakati alipokuwa United.
Licha ya kubeba makombe, Antonio Valencia alitwaa tuzo mbalimbali ikiwemo ya Mchezaji bora wa msimu, goli bora la msimu na mchezaji bora wa msimu aliyechaguliwa na wachezaji wenzake katika msimu wa 2011/12 na 2016/17.

Safari ya unahodha wa United ilianza kwenye mchezo wa fainali ya Europa dhidi ya Ajax 2017. Baada ya mchezo ule, Valencia alikabidhiwa rasmi kitambaa cha unahodha wa Man United baada ya Wayne Rooney kuondoka Old Trafford.
Tarehe 12 May, 2019. Valencia aliondoka United akiwa ameitumikia klabu hiyo kwa michezo 339 na kupachika magoli 29. Alirejea nyumbani kwao (Equador) kukipiga katika klabu ya LDU Quito kabla ya kujiunga na klabu ya Queretaro ya nchini Mexico ambapo amestaafia huko.
Hii ndiyo burudani yenye ushindi! Ingia kwenye kasino ya Meridianbet kufukuzia ushindi huu. Cheza sasa Lucky Lucky na uwe moja ya washindi na Mabingwa.
Big up kwake
Amecheza kwa mafanikio ni muda wa kupumuzika.
Hongera kwake
Apumzike tu
Hongera zake sasa apumzike
Jembe la united
Ampumzike tu
Amefanya vema
Hongera yake
Safii
Hongera yake
Wamefanya kazi nzuri sana mda wao wa kupumzika
Akapumzike Sasa Ili aendelee na maisha mengine
Safii
Vizur
Hongera yake
Kila la kheri