Ripoti zinaeleza kuwa nahodha wa Inter Milan, Lautaro Martínez, atapewa nafasi ya kucheza sambamba na Lionel Messi kuongoza safu ya ushambuliaji ya Argentina dhidi ya Cape Verde katika mechi ya Taji la Dunia itakayochezwa usiku wa leo.

Washindi wa mechi hii watakutana na mmoja kati ya Australia au Misri katika hatua ya 16 bora.
Argentina ndio mabingwa watetezi wa Taji la Dunia na miongoni mwa timu zinazopigiwa upatu mkubwa kutetea taji lao katika mashindano haya yanayofanyika Marekani, Canada na Mexico, baada ya kuziondoa Algeria, Austria na Jordan.
Hadi sasa, Argentina imekuwa ikitegemea sana mabao ya nyota wake Lionel Messi, ambaye anatarajiwa kuanza tena leo usiku katika uwanja wake wa nyumbani akiwa klabuni Inter Miami.
Kulikuwa na mashaka iwapo Lautaro Martínez angeendelea kubaki kwenye kikosi cha kwanza au angeachia nafasi mshambuliaji wa Atlético Madrid, Julián Álvarez.
Kwa mujibu wa TyC Sports, kocha Lionel Scaloni ataendelea kumchagua nahodha wa Inter Milan, ambaye alifunga penalti katika ushindi wa 3-1 dhidi ya Jordan na ameanza kila mechi hadi sasa.



