Arsenal wameripotiwa kuwa karibu zaidi na kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa Sporting Lisbon Tiago Tomas kwa mkataba wenye thamani ya pauni milioni 20.
Mchezaji huyo wa miaka 18 alifanikiwa kuingia kikosi cha kwanza kwa miamba wa Ureno msimu huu na amecheza mara kwa mara kwa upande timu yake ikifanya poa na kuwa kileleni mwa jedwali la Primeira Liga.
Kwa mujibu wa The Sun, mkurugenzi wa michezo Edu amekuwa akiwasiliana moja kwa moja na mkurugenzi wa mpira wa miguu Hugo Viana juu ya mpango wa kumsaini Tomas wakati akimfuatilia fowadi huyo kwenye mechi yao dhidi ya Benfica, ambao Gunners watakutana nao kwenye Ligi ya Europa Alhamisi ijayo.
Kijana huyo hivi karibuni alisaini kandarasi mpya, ilikuwa Juni 2020, kandarasi inajumuisha kifungu cha kununuliwa kwa mkataba kwa thamani ya pauni milioni 52.
Hata hivyo, kwa sababu ya hali ya kifedha ya sasa na matumizi ya Sporting kwa miaka michache iliyopita, inaeleweka kuwa kilabu hii ya Ureno inaweza kukubali dau la chini ya £20m.
Edu pia ameuambia uongozi wa Arsenal kwamba anaamini kilabu itajuta kumkosa mchezaji huyo mahiri.
Tomas amecheza mara 25 kwenye mechi za mashindano yote hadi sasa msimu huu, akifunga mabao matano na kutoa asisti tatu.
Unaweza kuvuna mkwanja mrefu kadiri uwezavyo kupitia mchezo wa Gold n Rocks kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Ni rahisi! Vigezo na masharti, kuzingatiwa.
Magdalena
Safi Sana arsenal mmefanya vyema
Caroline
Asante kwa taarifa
Dorophina
Nice update
Adelta
Arsenal yuko vizuri
Sania
Vizur sana Arsenal
Rahma
Safi sana Arsenal
Hopemwaikuka
Habar nzur hii
Sarah
Vizuri sana Arsenal
Mwanahamisi
Asante kwa taalifa
Sadick
Tatizo la Arsenal si kusajiri bali ni zaidi ya hapo
Lydia Emmanuel Magoti
Habari ikopoa
Neema juma
Arsenal wametisha kinyamaaa
Ernest Kimeru
Habari nzuri kwa Arsenal
Angelina
Nice
warda
Itakuwa poa