Klabu ya Arsenal msimu huu imeanza vyema sana msimu katika miavhuano yote, ambapo kwenye EPL ndio wanaongoza ligi lakini pia kwenye michuano ya Uropa wanaongoza kundi A wakiwa na pointi 12.

Bao la Granit Xhaka liliihakikishia Arsenal kufuzu kwa hatua ya mtoano ya michuano ya Uropa hapo jana akiwa amebakiza michezo miwili huku bao hilo lilifungwa dakika ya 71 ya mchezo dhidi ya PSV ya Uholanzi.
Mikel Arteta alichagua kikosi chenye nguvu huku Arsenal wakitafuta kuhakikisha wanasonga mbele kutoka Kundi A siku ya Alhamisi, lakini PSV ilionekana kuwa na uwezekano wa kuwafanya kusubiri baada ya kuonyesha uthabiti wa kujilinda.
Wakati Arsenal sasa wakiwa na uhakika wa kufuzu kwa hatua ya mtoano ya Ligi ya Uropa, pointi moja katika mechi ya marudiano wiki ijayo itawahakikishia nafasi ya kwanza na kufuzu kwa hatua ya 16 bora ya michuano hiyo.

Arsenal walianza kampeni yao ya Ligi ya Europa kwa ushindi mara tatu mfululizo kwa mara ya tano katika misimu mingi zaidi ya mashindano hayo. Katika moja ya matukio hayo ya awali, The Gunners walishinda mchezo wao wa nne wa kundi mnamo 2020/2021.
Wikendi hii, vijana wa Mikel Arteta kwenye Ligi kuu ya Uingereza watashuka dimbani kumenyana dhidi ya Southampton wakiwa ugenini huku matarajio yao msimu huu yakiwa ni kubeba ubingwa.


