Arteta: Mashabiki ndio Chachu ya Ushindi

Mikel Arteta Kocha Mkuu wa Arsenal amesema kuwa uwepo wa mashabiki kwenye mchezo wao wa Europa League dhidi ya Rapid Wien ndani ya Uwanja wa Emirates umewapa nguvu kuibuka na ushindi huku mashabiki waliojitokeza wakitaka jina la Mesut Ozil kurejeshwa ndani ya timu hiyo.

Awali mashabiki walikuwa wamezuiwa kuingia ndani ya Uwanja kutokana na kuchukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona jana waliruhusiwa mashabiki 2,000 ambao waliingia na mabango yaliyoandikwa arejeshwe Ozil mwenye miaka 32 baada ya jina lake kutolewa kwenye orodha ya wachezaji watakaocheza ndani ya Ligi Kuu England pamoja na Eropa League.

Mabao ya Arsenal wakati ikiibuka na ushindi wa mabao 4-1 yalifungwa na Alexandre Lacazette dk 10, Pablo Mari dk 18,Eddie Niketiah dk 44 na Emile Smith Rowe dk 66 lile la Rapid Wien lilipachikwa na Koya Kitagawa dk 47.

Ushindi huo unaifanya Arsenal kuweka rekodi yake ndani ya Europa League ikiwa imeshinda mechi zote tano na kujikusanyia pointi 15 nafasi ya kwanza kibindoni huku Rapid Wien ikiwa nafasi ya 3 na pointi 6 Kwenye kundi B.

Arteta amesema:”Mashabiki walitupa nguvu na kuwafanya wachezaji wapambane kwa juhudi kupata matokeo chanya hili ni jambo la faraja kwetu na mashabiki,”


FURAHIA MUZIKI MTANDAONI HUKU UKITENGEZA MKWANJA!!

Mchezo wa Astro Legend unakupatia burudani ya muziki kupitia kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!

INGIA MCHEZONI

20 Komentara

    Habari njema

    Jibu

    Nikweli kabisa

    Jibu

    Ni kweli kabisa

    Jibu

    Ni kweli mashabiki ndio wanawapa hamasa wachezaji na mpira unachangamka

    Jibu

    Haina kupinga hiyo ni kweli kabisa

    Jibu

    Ni habari nzuri

    Jibu

    Ndo mpango mzma

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Yess

    Jibu

    Kweli mashabiki ndo wanatia hamasa ya kucheza kwa bidii

    Jibu

    Arteta ni moto

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Asante kwa taarfa

    Jibu

    mmmh

    Jibu

    Ni Kweli kabisaaa

    Jibu

    Kwa kweli mashabiki wanaleta hamasa usajani

    Jibu

    Kwa kweli mashabiki wanaleta hamasa uwajani

    Jibu

    Mashabiki ndo mpango mzima

    Jibu

    Kwer kabisa

    Jibu

    Mashabiki wanamtaka OZIL Lakin Ozil mwenyewe hawezi kukubali tena kurudi

    Jibu

Acha ujumbe