Aubameyang Kuwakosa Man City.

Arsenal wanaendelea kutaabika kwa kupata matokeo mabaya kwenye EPL. Kuelekea mchezo wa robo fainali ya Carabao Cup, Aubameyang atakosekana kwenye mchezo huo.

Arsenal watawakaribisha Manchester City katika dimba la Emirate Stadium siku ya Jumanne usiku katika mchezo wa hatua ya robo fainali ya Carabao Cup.

Timu hizi zinakutana kwa mara nyingine mwaka huu zikiwa ni siku chache tangu walipocheza mchezo wa fainali ya FA Cup na Arsenal kuibuka kidedea. Ulikuwa ni wakati wa neema kwa Arsenal baada ya kubeba taji la FA, Community Shield na nahodha wao – Pierre -Emerick Aubameyang akasaini mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia klabu hiyo.

Tangu walipocheza mchezo wa mwisho, maisha yamebadilika sana kwa vilabu vyote viwili. City amekuwa na matokeo ya kupanda na kushuka wakiwa nafasi ya 7 kwenye msimamo wa EPL.

Pierre – Emerick Aubameyang akiwa na kombe la FA baada ya kuwaburuza Man City kwenye fainali.
Aubameyang anaiongoza Arsenal ambayo wameendelea kuwa na matokeo mabovu tangu kuanza kwa msimu huu na sasa wanashikilia nafasi ya 15 kwenye msimamo wa EPL wakiwa na pointi 14 katika michezo 14 waliyocheza mpaka sasa.

Kuelekea mchezo wa Carabao Cup, Mikel Arteta amethibitisha kukosekana kwa Aubameyang ambapo atakuwa anakosekana kwa mara ya pili mfululizo (hakuwepo kwenye mchezo dhidi ya Everton wikiendi iliyopita).

Auba alikuwa anajisikia vizuri zaidi jana kuliko siku mbili zilizopita. Atafanyiwa tena vipimo siku chache zijazo, baada ya hapo tutaona atachukua muda gani kurejea kikosini.

“Tunajua anaumuhimu kiasi gani kwetu na anayabeba majukumu hayo na anajitahidi kurejea kwenye ubora wake mapema awezavyo. Auba hayupo tayari kwa mchezo wa kesho, huo ni uhalisia.

“Kesho hatocheza, tutaangalia nani anapatikana kwasababu bado tunamashaka na baadhi ya sehemu zingine pia. Tunahitaji kupata muunganiko wa timu yenye ushindani kwa sababu tunajua viwango walivyonavyo City na tunahitaji kushinda mchezo wa kesho.” Alisema Arteta.

Kukosekana kwa Auba pengine kutamlazimu Arteta kupanga kikosi chenye wachezaji chipukizi wengi ili kuendana na kasi ya mechi zinazofuata kuelekea mwezi Januari 2021.


VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!

Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini???

SOMA ZAIDI

15 Komentara

    Get well soon Auba

    Jibu

    Arsenal sijui wanakwama wap

    Jibu

    Arsenal wanatakiwa waongeze juhudi ili waweze kurejea kwenye kiwango

    Jibu

    Arsenal msimu huu sijui inakuaje

    Jibu

    Auba ni moto

    Jibu

    Du ni mbona hatari

    Jibu

    Arsenal cjui tatizo nn tena

    Jibu

    Duu sio poa

    Jibu

    Sio sawa

    Jibu

    Dhuuu nomaa

    Jibu

    Arsenal msimu huu sijui inakuaje

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Pigo kwa Arteta

    Jibu

    Pigo kwa arsenal

    Jibu

    Ndo hivyo tena haina jinsi

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.