Mchezaji wa kimatifa kutokea Gabon Aubameyang amekamilisha amekamilisha usajiri wake na klabu ya Barcelona baada ya kuvunja mkataba na klabu yake ya Arsenal na miamba hiyo ya jiji la Barcelona wamemtangaza rasmi leo jumatano.
Kulingana na mkataba aliosaini wa kumuweka kwenye klabu hiyo mpaka june 30 2025 na kuna kipengere cha kumwacha mwaka 30 june 2023, huku pia kukiwa na kipengere cha kuuzwa kwa 100 million euro ikiwa kuna klabu itajitaji huduma yake.

Aubameyang alisajiriwa na klabu ya Arsenal akitokea nchini Ujerumani kwenye klabu ya Borussia Dortmund, amabako alifunga magoli 141 kwa misimu yake minne na nusu aliyotumia kwenye klabu hiyo, huku mwaka 2017 alikuwa mfungaji bora nchini humo huku akifunga magoli 31.
Aubameyangameifungia klabu ya Arsena magoli 92 kwenye michezo 163 kati ya mwaka 2018 hadi 2022, amezichezea klabu kama AC Milan, Dijon, Lille, Monaco, na Saint-Etienne, pia ameicheza timu ya taifa Gabon michezo 72 na kufunga magoli 30.
Dakika tano pekee zinakutosha kuwa mmoja wa washindi wa mkwanja mrefu ndani ya kasino pendwa ya meridianbettz katika sloti maridhawa ya KENO, moja ya michezo inayoipa thamani dau lako.


