Australian Open : Rafael Nadal Atinga Fainali.

Mcheza Tennis namba 5 kw aubora duniani, Rafael Nadal ameshinda mtihani mkali kutoka kwa Matteo Berrettini na kufika fainali yake ya sita ya Australian Open mjini Melbourne, Australia.

 

Nadal, 35 bado yuko mbioni kushinda taji la 21 la Grand Slam mjini Melbourne na taji lake la kwanza la Australian Open tangu 2009. Mpaka mapumziko akiwa mbele kwa seti 4-3 na kumsaidia Mhispania huyo kupata ushindi wa 3-6 2-6 6-3 3-6.

Mchezaji huyo ametinga fainali akimsubiri mshindi kati ya Stefano Tsitsipas au Daniil Medvedev katika fainali itakayopigwa Jumaapili.

“Ina maana kubwa kwangu kuwa katika fainali tena hapa,” Nadal alisema akitabasamu.

“Kwangu mimi, yote yanahusu Australian Open zaidi ya kitu kingine chochote. Ni tukio la kushangaza tu ambalo nimekuwa na bahati mbaya [kwa] kutokana na majeraha katika taaluma yangu.

“Pia, nimecheza fainali za kushangaza nikiwa na nafasi nzuri dhidi ya Novak Djokovic mnamo 2012 na Roger Federer mnamo 2017, nilikuwa karibu mara kadhaa.

“Nilikuwa na bahati sana kushinda mara moja katika taaluma yangu na sikuwahi kufikiria kuwa na nafasi nyingine 2022, kwa hivyo nitajaribu tu na kufurahia ushindi leo kisha nijaribu tu niwezavyo.” aliongeza.


VUNA MKWANJA NA KENO

Dakika tano pekee zinakutosha kuwa mmoja wa washindi wa mkwanja mrefu ndani ya kasino pendwa ya meridianbettz katika sloti maridhawa ya KENO, moja ya michezo inayoipa thamani dau lako.

tetesi, Tetesi za Soka barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe