Klabu ya Azam FC, kupitia uongozi wao uedhibitisha kwamba wamejiandaa na wako tayari kupambana katika mchezo wao ujao wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi Pyramid kutokea Misri.
Azam FC wanatarajiwa kuvaana na Pyramid Oktoba 16, mwaka huu katika mchezo wa hatua ya kwanza ya michuano hiyo ambapo wataanzia nyumbani kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar.
Katika hatua ya awali Azam FC iliwaondosha Horseed ya Somalia kwa jumla ya mabao 4-1, wakishinda mabao 3-1 mchezo wa kwanza na bao 1-0 waliporudiana.
Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano ya klabu, Zakaria Thabith alisema: “Sehemu ya wachezaji ambao hawajaitwa kwenye vikosi vya timu zao za taifa inaendelea na mazoezi yaliyoanza tangu Jumanne wiki iliyopita, ili kujiandaa na ratiba ya michezo iliyo mbele yetu.
Mchezo wetu ujao ni ule wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Pyramid FC ya Misri. Kocha mkuu George Lwandamina anajua ubora wa wapinzani wetu lakini nasi tunajiamini na tupo tayari kupambana kuiwakilisha vyema nchi yetu.
Fanya wiki yako iwe ya kuvutia zaidi, tunaelekea Los Angeles kutengeneza mkwanja na kasino maridhawa ya LA Rouge kutoka katika kasino za mtandaoni za meridianbettz, Fursa ya kufurahi huku unajaza pochi yako.
CHEZA HAPA