Bila shaka wapenzi wa Man City pamoja na klabu yao watakuwa hawaamini kilichotokea, walipokutana na mabingwa wa Hispania kwenye Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Real Madrid walikuwa na matumaini hafifu zaidi kuweza kutoboa kufika fainali baada ya kuruhusu kichapo cha 3-2 kwenye mechi ya kwanza ya nusu fainali. Hapa Man City wakuwa na shughuli ya kumalizia kazi tu!
Dakika ya 73 ilipoteza zaidi matumiani ya Real baada ya Man City kupata goli lao la kwanza, lakini dakika ya 90 na 91 ilihrejesha matumaini ya Real Madrid kupitia magoli ya Rodrygo. Kisha Benzema akamaliza kwenye kipindi cha nyongeza.
Kufuatia kipigo hicho na kuondolewa kwenye Ligi ya Mabingwa, wakisalia Liverpool na Real Madrid wanaokutana kwenye fainali, Pep Guardiola anasema kuwa wanahitaji muda wa kutafakari kichapo hicho.
“Ndiyo, tulikuwa karibu sana, lakini mwishowe tumeshindwa kufikia. Tulikuwa vizuri sana kipindi cha kwanza na hatukusumbuka sana. Baada ya kupata goli tulikuwa bora zaidi, tulipata chimbo letu na wachezaji walicheza kwa starehe.” – Pep Guardiola
“Hatujasumbuka sana, lakini tumejitahidi, hiyo ni kawaida. Ni nusu fainali na wachezaji wanaweza kuhisi presha. Soka halitabiriki, wakati mwingine unatakiwa kukubali tu. Sasa tunahitaji muda kufikilia hili na kurejea nyumbani.” – Pep Guardiola
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.