KOCHA Mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi amefunguka kuwa kuelekea katika mchezo wao dhidi ya Simba amewataka mabeki wake akiwemo, Yannic Bangala na Bakari Mwamnyeto kuongeza umakini zaidi kwa washambuliaji wa Simba kuhakikisha hawapati nafasi ya kuwadhuru.
Akizungumza na Championi Jumatano, Nabi alisema kuwa amewataka mabeki wake akiwemo Yannic Bangala kuongeza umakini katika mchezo huo juu ya washambuliaji wa Simba kwa kuhakikisha hawapati nafasi ya kuwadhuru kwa namna yoyote.
Yanga anaingia kwenye mchezo huo akiwa anaongoza kwa pointi 54 akifuatiwa na Simba wenye pointi 41, huku wakiwa na mchezo mmoja mkononi ambao bado hawajaucheza.
Yanga na Simba zinatarajia kucheza Jumamosi ya Aprili 30 Uwanja wa Benjamin Mkapa Dar.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.