Barcelona Kuwapiku Real kwa Pablo Torre

Kwa mujibu wa Mundo Deportivo, Barcelona tayari wana makubaliano na nyota wa Racing Pablo Torre. Taarifa zinasema Makubaliano ya kumsaini kinda huyo mwenye umri wa miaka 18 yamekamilika, sasa kilichobaki ni Barcelona kufanya makubaliano na klabu yake.

Barcelona wameipiku Real Madrid, ambao pia walikuwa na nia ya kumsajili kinda huyo. Kiungo mbunifu anayeweza kucheza katikati au upande wa kushoto, mkataba wake utadumu hadi 2025.

Barcelona Kuwapiku Real kwa Pablo Torre

Tayari amekuwa mtu muhimu kwa Racing, ambao kwa sasa wako vinara wa Kundi 1 la Ligi Daraja la Tatu la Uhispania. Amecheza mechi 21 msimu huu, akianza mara 18, na amefunga mabao sita.

Namna Barcelona walivyoishinda Madrid kumsajili Torre inawakumbusha jinsi walivyo wakwamisha wapinzani wao wakubwa kumsajili Pedri kutoka Las Palmas mwaka 2019. Alikaa Visiwa vya Canary kwa mkopo hadi majira ya joto ya 2020.


KASINO YA MTANDAONI: EMOTICOINS SABABU YA KUVUNA ZAIDI.

Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.

senegal, Senegal Mabingwa AFCON 2021., Meridianbet

CHEZA HAPA.

Acha ujumbe