Barcelona Yawanyatia Aguero na Alaba.


Klabu ya Barcelona ya Uhispania wanatumai wanaweza kumnasa Sergio Aguero na David Alaba kwa uhamisho wa bure msimu huu wa joto baada ya mikataba yao kumalizika huko Manchester City na Bayern Munich kama ilivyoainishwa.

Aguero anatarajiwa kuondoka Etihad baada ya miaka 10 ambayo imemwona kuwa mfungaji bora wa muda wote wa kilabu akiwa na mabao 256 na kuinua mataji manne ya Ligi Kuu ya Uingereza.

 

Walakini, majeraha tangu hapo yamemkuta mchezaji huyo mwenye miaka 32 na sasa ametimiza mwaka mzima bila kufunga bao la Ligi Kuu pale Etihad.

Alaba pia aliweka wazi kwamba hawawezi kuongeza mkataba na waajiri wake wa sasa, Bayern Munich baada ya kudumu kwa kipindi cha muda mrefu.

Barcelona inaangalia uwezekano wa kuwanasa wachezaji hao bila malipo (huru) mara kandarasi zao zitakapo kamilika katika majira ya kiangazi.

Ukiachana na Balcelona vilabu kama Real Madrid, Manchester United, PSG, Chelsea na Liverpool zimeonyesha nia ya kuwanasa wachezaji hao.


USHINDI UPI NI MKUBWA KWAKO, £2,000,000? 🤑

Pokea mualiko wa Meridianbet na Pragmatic Play kutengeneza mkwanja kwenye kasino ya mtandaoni sasa. Jiunge sasa kupata ishindi huu.

INGIA MCHEZONI

14 Komentara

    Wafanye mpango wamchukuwe kijana Yuko vizuri

    Jibu

    Alaba yuko vizuri

    Jibu

    Barca watulie hawana maajabu sasa

    Jibu

    Alaba namkubali

    Jibu

    Barca wakiwapata miamba hao wawili wataenda kuisaidia klabu

    Jibu

    Aguero yupo juu

    Jibu

    Wazo la kumvuta Aguero Barca ni la kushangaza sana kwani Barca inahitaji kurudisha heshima yake kwenye ulimwengu wa soka lakini Karata yao kwa Aguero ni kazi bureeeee

    Jibu

    Aguero yuko makini

    Jibu

    Wanafaa sana

    Jibu

    Wapo vizuri

    Jibu

    Wote wako vizuri

    Jibu

    Barca wakimpata Alaba itakuwa poa sana

    Jibu

    Alaba Yuko poq

    Jibu

    Wapo vizuri

    Jibu

Acha ujumbe