Benzema Akamilisha Uhamisho Kwenda Kwa Vinara wa Ligi ya Saudi (RSL), Al Hilal

Mshindi wa ubingwa wa Ligi Kuu ya Saudi (Roshn Saudi League), Karim Benzema, amejiunga na Al Hilal akitokea Al Ittihad kwa uhamisho huru.

Benzema Akamilisha Uhamisho Kwenda Kwa Vinara wa Ligi ya Saudi (RSL), Al Hilal

Mfaransa huyo, ambaye ni Mchezaji Bora wa Msimu wa sasa wa mashindano hayo, alikamilisha uhamisho huo siku ya mwisho ya dirisha la usajili la majira ya baridi, lililofungwa Jumatatu usiku.

Benzema amesaini mkataba wa mwaka mmoja na nusu na vinara wa sasa wa RSL, ambao wanaongoza msimamo wa ligi kwa tofauti ya pointi moja dhidi ya Al Nassr.

Meridianbet inakwambia kuwa endelea kubashiri hapa kwani ODDS KUBWA na machaguo zaidi ya 1000 yapo hapa. Ingia kwenye akaunti yako na uanze safari yako ya ushindi sasa.

Baada ya kujiunga na Al Ittihad mwezi Juni 2023, Benzema aliiongoza klabu ya Jeddah kutwaa mataji mawili msimu uliopita, akishinda RSL na Kombe la Mfalme. Alifunga mabao 21 katika ligi kuu ya Saudi pekee, akimaliza nafasi ya tatu kwenye mbio za kiatu cha dhahabu, nyuma ya Ivan Toney (23) na mshindi Cristiano Ronaldo (25).

Benzema Akamilisha Uhamisho Kwenda Kwa Vinara wa Ligi ya Saudi (RSL), Al Hilal

Kwa ujumla, Benzema amecheza mechi 64 katika RSL, akifunga mabao 38. Msimu huu amepachika mabao nane katika mechi 14.

Al Hilal watashuka dimbani tena Alhamisi ijayo, wakisafiri kwenda kuwakabili Al Okhdood walioko nafasi ya pili kutoka mkiani katika mzunguko wa 21 wa ligi. Cha kuvutia, Benzema alifunga hat-trick mara ya mwisho alipokutana na klabu hiyo jijini Al Najran, katika raundi ya ufunguzi wa msimu wa 2025–26.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.