Bingwa Rudisha Nje kwa Wiki 16!

Mshindi mara mbili wa michuano ya Olympic na ambaye anashikilia rekodi ya kushinda kukimbia mbio za umbali wa 800m duniani, David Rudisha atakaa nje ya uwanja kwa muda wa majuma 16! Hii imetokana na yeye kuumia kifundo chake cha mguu wa kushoto.

Mwanamichezo huyo mwenye umri wa miaka 31 aliumia sehemu hiyo ya mwili wake akiwa kijijini kwao Kilgoris, magharibi mwa taifa la Kenya siku ya tarehe 19 mwezi Mei ambapo madaktari wake wanasema kuwa uchungizi wa karibu zaidi uligundua kuwa amepasuka kifundo cha mguu.

“Hatukuweza kufanya upasuaji kumtibu ambapo sasa mchezaji huyo atakuwa chini ya uangalizi maalum kwa siku moja inayofuata,” aliyasema hayo Victor Bargoria, ambaye ni mtaalam wa upasuaji, akiwaambia AFP, akaongezea kuwa itamchukua muda wa wiki 16 kwa mchezaji huyo kuanza tena mazoezi yake.

Rudisha, ambaye ameshinda rekodi ya 2012 London Olympics kwa muda wa saa 1:40.91, alikuwa anatarajiwa kurudi tena uwanjani baada ya kuwa ameumia goti ambapo ilimzuia kabisa kuchuana katika mashindano ya ubingwa wa dunia huko Doha mwezi Septemba.

Rudisha alikosa kushiriki michezoni kati ya mwaka 2013 pamoja na mwaka 2014 ikiwa ni matokeo ya kuumia mguu wake. Tunamtakia heri apone haraka!

39 Komentara

    Rudisha bonge la mwanariadha#meridianbettz

    Jibu

    Jamaa anatisha sanaa Yani hatari

    Jibu

    Kushikilia hiyo record mfululizo sio kitu kidogooo…tumuombee apone haraka

    Jibu

    Jamaa yuko vizuri san

    Jibu

    Pole sana mungu akupe afya upya urudi kambini

    Jibu

    Tunamtakia heri apone haraka

    Jibu

    Pole yake tunaomba apone haraka

    Jibu

    Pole bingwa Rudisha ,mungu akusaidie upone urudi kutumikia taifa.

    Jibu

    Apone aje andelee kutumikia taifa

    Jibu

    Pole sana atarud kama zamani

    Jibu

    Rudisha noma sana kweny liadha

    Jibu

    Pole sana..!bonge la mwanaliadha utarudi kama zamani

    Jibu

    mungu akupe afya urudi kambini

    Jibu

    Jamaha yupo vizuri huyo kwenye rihaza

    Jibu

    Pole sana kinaja, tunakutakia upone haraka

    Jibu

    Mwanariadha mahili

    Jibu

    so sad kwa rudisha

    Jibu

    Pole sana wiki kumi na sita sio nyingi sana atarudi tuu

    Jibu

    Yupo vizuri Sana mungu amjalie arudi dimbani

    Jibu

    Pole sana kwake

    Jibu

    Pole sn kjana

    Jibu

    Pole yake

    Jibu

    Pole Sana kwake atakaa sawa soon

    Jibu

    Mwanaliaza mzuri sana

    Jibu

    Mwenyez amsaidie

    Jibu

    Mungu amsaidie atapona

    Jibu

    Jamani pole yake#Meridianbettz

    Jibu

    Rudisha habari nyngne

    Jibu

    Pole yake jamani

    Jibu

    Rudisha yuko vizur sana

    Jibu

    get well soon

    Jibu

    Rudisha bonge la mwanariadha#meridianbettz

    Jibu

    Mungu amponye#meridianbettz

    Jibu

    Duh mungu atamsaidia

    Jibu

    Pole sana mungu atakusaidia#meridianbettz

    Jibu

    Mungu atamponya na atarudi ulingon

    Jibu

    Get well soon 🙏🙏

    Jibu

    Rudisha yupo vzr kwny kukimbizah upepo kila la heri atapona kwa uwez wa mungu🙏🙏🙏🙏🏼

    Jibu

    Pole yake sana

    Jibu

Acha ujumbe