Gleison Bremer amekubali kusaini mkataba mpya wa muda mrefu na Juventus ambao utajumuisha kifungu cha juu cha kutolewa kuliko mkataba wake wa sasa.
Beki huyo wa kati wa Brazil mwenye umri wa miaka 27 aliweka hati hati juu ya mkataba mpya wa miaka minne na Bibi Kizee mnamo Desemba mwaka jana, makubaliano ambayo yalijumuisha kifungu cha kutolewa cha €60m. Kuelekea majira ya joto, uvumi ulianza kuzunguka juu ya mustakabali wake huko Turin.
Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.
Vilabu kadhaa kote barani Ulaya ikiwa ni pamoja na Manchester United vilikuwa na nia ya kutaka kumsajili Bremer msimu huu wa joto, lakini uhamisho huo haukutimia. Ilionekana wazi kuwa beki huyo alifurahishwa na Juventus na hakufanya jaribio lolote la kutaka kuondoka.
Calciomercato.com na Fabrizio Romano wanaeleza jinsi Bremer amekubali kusaini mkataba mpya wa muda mrefu na Juventus, mkataba ambao una kipengele cha juu zaidi cha kuachiliwa kuliko €60m aliyonayo sasa. Kandarasi itasainiwa saa zijazo, kuthibitisha maisha yake ya baadaye na Bibi Kizee.
