Gianluigi Buffon alishabainisha kuwa hatakuwa akiendelea kuchezea Juventus, anatarajia kutemana na miamba hao wa Italia, lakini hakubainisha ikiwa huo ndiyo utakuwa mwisho wake wa soka.
Ripoti zinadai kuwa golikipa huyu mwenye miaka 43 ataendelea kuichezea Barcelona baada ya kumalizana na Juve, na Barcelona tayari wameshampa dili hilo.
Kwa mujibu wa Footmercato, ukiachana na Buffon kufikiria kustaafu, chaguo jingine litakuwa ni kuendelea na Barcelona na tayari wameshaanza kufanya mawasiliano juu ya hilo.
Barcelona ni moja kati ya klabu tatu, wakiwa pamoja na Juventus na Real Madrid ambao bado hawatangaza kujiondoa kwenye mradi wa Super League, wakati Juventus akionekana atalazimika kujiondoa ikiwa anahitaji kushiriki Serie A.
Hivyo, klabu zote zinatazamia kupata hamisho za bei nafuu sokoni wakati dirisha la usajili likiwa wazi, na kwa Buffon anaonekana kuwa chaguo mahsusi kwa Barcelona. Hata hivyo, Barcelona pia wanatarajiwa kumuuza Neto na kuongeza fedha kidogo za kufadhili biashara hii.
Hii ndiyo burudani yenye ushindi! Ingia kwenye kasino ya Meridianbet kufukuzia ushindi huu. Cheza sasa Lucky Lucky na uwe moja ya washindi na Mabingwa.
Aende tuu barc
Apumzike tu#meridianbett
Buffon ni bora arejee barca
Kazi na umri kama vip apumzike
💥💥
Aende tu
Astaafu tu
Aende tuu
Aende tuu
Vizuri