Cabaye: Sitaki Kustaafu

Yohan Cabaye anasema kuwa anataka kuendelea kucheza soka hata mara baada ya kumalizika kwa mkataba wake klabuni Saint-Etienne.

Mkataba wake unafikia ukomo ifikapo tarehe 30 Juni mwaka huu na anataka kuwa na Les Verts ama kwingine kokote.

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 34 ni mshindi mara mbili akiwa na LOSC mwaka 2011 na bingwa wa Ligue 1 Conforama akiwa na klabu ya soka ya PSG mwaka 2014 na mwaka 2015, alicheza mara 12 kwa ajili ya klabu ya soka ya Saint-Etienne katika msimu ambao alikumbwa na majeraha na kisha ikafuatiwa na janga la Covid-19.

Cabaye aliwaambiwa L’Equipe: “Ninataka kuendelea kucheza soka na sitaki kabisa kusikia habari za kustaafu kwangu. Wakati huu ambao haturuhusiwi kucheza nimejipima na kuona kwamba hali yangu katika soka ikoje. Ninaikumbuka sana michezo yetu ya mpira wa miguu.

Imenifanyia mema mengi sana. Kutoka katika kujiwazia mimi mwenyewe hadi mpaka kufikia kucheza soka la kiushindani haswa, kuona soka la ushindani la wikiendi iliyopita huko Bundesliga, hata kama ikichezwa bila ya uwepo wa mashabiki basi ule utaratibu wa mwanzo wa asili utapotea kabisa. Ninataka kucheza soka. Iwe ni pale Saint-Etienne ama kwingine kokote kule. Mkataba wangu unafikia ukomo ikifika mwezi Juni 30 mwaka huu na hakuna ambalo limeamuliwa kati yetu mpaka sasa hivi.”

Klabu ya soka ya Saint-Etienne imepangwa kumenyana na klabu ya zamani ya Cabaye, PSG katika hatua ya fainali ya kuwania kombe la Coupe de France lakini haipo wazi endapo mchezaji huyo wa kimataifa wa taifa la Ufaransa ataendelea kuwa katika klabu yake wakati fainali ikifika.

Mchezaji Cabaye alisema: “Kocha Claude Puel aliongea nami kuhusu kuongeza mkataba wangu klabuni hapo na kisha akaongelea suala hilo mbele ya jamii yote. Tupo katika mazungumzo kwa sasa na sijafunga milango ya kusajiliwa tena ama kusaini mkataba mpya. Tutaangalia kitakachotokea kwetu. Kwa sasa sipingani na lolote lililo mbele yangu.”

38 Komentara

    Bado ana uwezo mzuri na maamuzi yake yako sahihi

    Jibu

    Cabaye ni bonge la Kiungo#Meridianbettz

    Jibu

    Jamaa mpira uko damuni cabaye yuko sahihi

    Jibu

    Cabaye Ni mchezaji mzuri sana

    Jibu

    Anajikongoja tu kutafuta pesa lakini kusema kweli just limezama

    Jibu

    Cabaye astaaf tu umri ushamtupa mkono maana majeruhi yamezidi bora apumzike

    Jibu

    Jamaa anaujua mpira huyo

    Jibu

    duuh

    Jibu

    Muacheni aendelee umri wake unaruhusu

    Jibu

    Anakosea kwasababu ni jambo la busara sana kama muda wako wa kustaafu umefika hlf ukatae kwasababu kuna wengine wanaihitaji hiuo nafasi hivo kama muda wakustaafu umefika basi ni vyema angeachia ngazi tuu awapishe wengine

    Jibu

    Anakosea kwasababu ni jambo la busara sana kama muda wako wa kustaafu umefika hlf ukatae kwasababu kuna wengine wanaihitaji hiyo nafasi hivo kama muda wakustaafu umefika basi ni vyema angeachia ngazi tuu awapishe wengine

    Jibu

    Cabaye ni mchezaji mnzur

    Jibu

    Duuuh

    Jibu

    Yohan cabaye ni bonge la kiungo ni Jambo la busara kuendeleah kukipgah iliawez kuwap uzoefu na kujifunza kwa wanao chipukiah kupitiah kwake thnks meridian kwa gud news

    Jibu

    Kama anauwezo mzuri aendelee kucheza

    Jibu

    Sio sawa kama muda wa kustaafu umefika ni bora afanye ivyo itakua busara Sana

    Jibu

    Mpira upo ndani ya damu..!ila unaweza kustaf theni uwe kocha kwenye timu ndogo ndogo ili wengine wajifunze kupitia wew..!

    Jibu

    Jamaa anajua Sana mpira

    Jibu

    Anaweza

    Jibu

    Kama umri unaruhusu aendelee

    Jibu

    Kuna maishaa baada ya mpira kama umri umekutupa mkono fanya mambo mengine

    Jibu

    waachie na wengine muda wako wa kustaafu umefika kampumzike

    Jibu

    Kuna maisha mengine kama umri wake umeenda afanye kingine

    Jibu

    Yupo vizuri Sana Ila umri ukisogea kustaafu ni lazima

    Jibu

    Umri umeenda aache tamaa..

    Jibu

    Kama bado ana nguvuu aendelee tu

    Jibu

    cabaye yuko vizuri sana

    Jibu

    Cabaye yupo sahihi

    Jibu

    Kiungo fundi# meridianbettz

    Jibu

    Asante kwa taarifa meridianbet.

    Jibu

    Cabaye bado yupo vizuri sanaaa

    Jibu

    Ahsant sana meridianbet kwa taarifa

    Jibu

    moja,ya kiungo bora wa chini lakini akikosea sana kwenda kucheza,ligi ya kwao

    Jibu

    Akipige tu ila kuna muda mpira utamkataa kulingana na umri

    Jibu

    Bado ana uwezo mzuri na maamuzi yake yako sahihi

    Jibu

    Umri unaruhusu mwacheni aende

    Jibu

    yupo vzr

    Jibu

    Asanteh kwa taarifa

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.