Shirikisho la kandanda barani Afrika CAF limetangaza kuwa kuanzia mwakani wapo kwenye majadiliano ya kuboresha kanuni katika mashindano ya CHAN ambayo yanahusisha wachezaji wanaocheza katika ligi za ndani pekee kuanzia mwaka 2009.
Kupitia rais wa CAF, Patrick Motsepe amesema wanaangalia uwezekano wa kuwajumuisha katika mashindano hayo wachezaji wanaocheza soka la kulipwa nje ya ligi zao lakini ndani ya Bara la Afrika.
Aviator, poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Piggy Party na mingine kibao upige pesa na Meridianbet. Ingia www. meridianbet.co.tz.
Motsepe anasema kanuni hiyo inalenga kuyaboresha zaidi mashindano hayo na kuziongezea timu shiriki kuwa na vikosi imara wakati wa mashindano.