Calafiori ni Mali ya Arsenal
Makala iliyopita
Zaniolo Ajiunga na Atalanta
Makala ijayo
Dili la Feisal Kwenda Simba Limekufa
Beki huyo wa kimataifa wa Italia mwenye umri wa miaka (22) amekua na msimu bora sana ndani ya ligi kuu ya Italia akiitumikia klabu ya Bologna ambapo alikua mchezaji muhimu ndani ya kikosi cha kocha Thiago Motta mpaka wanafanikiwa kufuzu ligi ya mabingwa barani ulaya.
Beki Calafiori atakua na msaada mkubwa sana ndani ya kikosi cha Arsenal ambapo ataongeza ubora katika safu ya ulinzi ya klabu hiyo, Kwani beki huyo ana uwezo wa kucheza nafasi zaidi ya moja uwanjani akicheza kama beki wa katikati lakini pia ana uwezo wa kucheza kama beki wa pembeni kushoto.