Kiungo mshambuliaji wa timu ya Simba SC, Clatous Chama amesema kuwa malengo yao msimu huu ni kufika fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika, hivyo Kaizer Chiefs wasitarajie mteremko katika mchezo wa kwanza wa robo fainali.
Jumammosi, Simba SC wanatarajia kushuka uwanja wa FNB Afrika Kusini kuwakabili wabishi Kaizer Chiefs, ambao wametinga hatua ya robo fainali wakitokea Kundi C.
Chama amesema pamoja na kufahamu kuwa mchezo hautakuwa mwepesi kwa kila timu, hawatakubali kupoteza mchezo huo.
“Tumekuja Afrika Kusini kutafuta matokeo ili kujiweka katika nafasi nzuri tutakaporudi nyumbani katika mchezo wa marudiano ambao ndio utatoa hatima ya nani aende nusu fainali.”
“Haikuwa jambo rahisi kumaliza nafasi ya kwanza mbele ya bingwa mtetezi, ambaye ni kinara katika orodha ya timu bora Afrika, tumekuja huku kupambana kila mchezaji kiu yake ni kuona tunacheza fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika,” alisema Chama
Chama aliongeza kuwa ubora wa kikosi chao unatokana na malengo waliyojiwekea na umoja uliopo, ambacho kimekuwa na muendelezo mzuri wa matokeo kuanzia katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara pamoja na Kombe la Shirikisho.
Hii ndiyo burudani yenye ushindi! Ingia kwenye kasino ya Meridianbet kufukuzia ushindi huu. Cheza sasa Lucky Lucky na uwe moja ya washindi na Mabingwa.
Saupha
Aendelee kukaza buti
Caroline
Asante kwa taarifa
Sania mapua
Simba daima mbele
Theonestina
Habari njema
Shakila
Good new
dorophina
Wakijitahidi watafanikiwa tu
aisha
Atakaebisha yeye mchawi
Magdalena
Kikubwa kujituma
Lydia Emmanuel Magoti
Safii simba wapambanaji
Mariam mtandama
Habar njema
Elika
Kaza mwendo kijana
Furahav
Simba hatari.
Sauda
Akaze tu
Angelina
Niceupdate
Sarah
Simba hatari