Hali sio shwari kunako klabu ya Chelsea. Matokeo ya siku za karibuni hayaendani na uwekezaji uliofanywa na Roman Abramovich.
Chelsea wamepoteza nafasi kadhaa za kuongoza msimamo wa EPL na matokeo ya sare dhidi ya Aston Villa yameishusha timu hiyo mpaka nafasi ya 6.
Frank Lampard ameambulia pointi 4 katika mechi 5 alizocheza siku za karibuni na hali imeanza kuwa mbaya klabuni hapo.
Licha ya kwamba timu hiyo imepoteza mchezo 1 kati ya 14 iliyocheza kwenye uwanja wake wa nyumbani, bado matokeo ya kikosi hicho hayaendani na uwekezaji wenye thamani ya takribani pauni milioni 220.
Lampard aliwasajili Ziyech, Werner, Mendy, Havertz, Thiago Silva na Chilwell kama sehemu ya kuboresha kikosi hicho lakini hali haijawa hivyo.
Kwan Lampard anakwama wapi? Timu hii inauwezo wa kutwaa ubingwa wa EPL msimu huu?
Mshambuliaji wa zamani wa timu hiyo – Chris Sutton amegusia hilo alipozungumza na BBC Radio 5. Sutton amesema “Kwa sasa ni klabu yenye matatizo kwa sababu wanacheza chini ya kiwango.
“Frank Lampard anapaswa kupata matokeo ya ushindi haraka iwezekanavyo, tofauti na hapo, kama tunavyojua, mambo huwa yanabadilika Chelsea.
“Sidhani kama Chelsea wanaweza kushinda ubingwa. Wanahitaji kurudi kwenye ubora wao kwanza.”
Lampard atamkaribisha Pep Guardiola kwenye mchezo dhidi ya Man City mapema mwezi Januari 2021.
VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini?
Angelina
Poleni sana chelsea kwa kipigo😀
Sarah
Pole yao chelsel
Shakila mrope
Poleni san Chelsea
Chiku
Ukianguka jipanguse Anza safari msikate Tamaa chelsea
Rahmal
Polen sana chelsea
Ernest Kimeru
EPL imekuwa na changamoto sana msimu huu kiasi kwamba timu zilizofanya usajili mkubwa makocha wao wapo katika pressure kubwa sana
Hopemwaikuka
Mambo yanazid kuwaendea kombo
Issa
Lampatd aangalie timu yake vizur
Neema juma
Naamini watakuwa fresh wasikate tamaa
Dorophina
Chelsea sijui imekuwaje msimu huu
Saupha mohamed
Chelsea mnakwama wapi
Lydia Emmanuel Magoti
Timu mbovu ishakuwa
Fatina mfingi
Chelsea mnazingua sanaa!
Mwanahamisi
Chelsea hawana jipya
Asia Abdy
Mambo yatakuwa sawa tu
warda
Ndo mchezo kesho unapanda kesho kutwa unashuka
Tatu
Chelsea sijui wanakwama wapi
Caroline
Chelsea mnatuangusha
Zahara omary
Chalsea mnazingua siku hizi
Sania
Poleni sana chelsea