Chelsea Yamgeukia Gabriel Slonina Kama Mrithi wa Kepa

Klabu ya Chelsea inam’nyemela golikipa wa klabu ya Chicago Fire inayoshiriki ligi kuu ya Marekani kama mbadala wa golikipa wa klabu hiyoo aliyesajiriwa kwa usajiri ulioweka rekodi kwenye klabu hiyo Kepa Arrizabalaga.

Golikipa huyo wa kimataifa wa Hispani Kepa Arrizabalaga amepanga kuachana na klabu hiyo kwenye dirisha hili la majira ya kiangazi, ili kuweza kupata nafasi ya kucheza mara kwa mara baada ya nafasi yake kuchukuliwa Edouard Mendy.

Klabu ya Real Madrid ilipeleka offa ya kutaka kumsajiri Gabriel Sloninan ilikataliwa na sasa Klabu ya Chelsea imengia kwenye kinyanganyiro hicho, ila mpaka sasa hakuna upande wowote kati uliothibitisha kuwa wapo kwenye mazungumzo.

Kepa msimu uliyoisha ameicheza klabu ya Chelsea michezo 15 kwenye mashindano yote, lakini amecheza mara moja tu baada kukosa penati kwenye mchezo wa Carabao Cup dhidi ya Liverpool ambao walipoteza mwezi February.

Pia kuna tetesi kuwa Thomas Tuchel amepanga kumpa mkataba mpya Mendy kwenye majira haya ya kiangazi, baada ya kuwa ni yeye ndio mchezaji pekee ambaye analipwa pesa ndogo kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo.


ALIYA’S WISHES

Bila shaka unatamani ushindi mkubwa, vipi kuhusu kujaribu Sloti hii ya Aliya’s Wishes? jaribu ushinde sasa.Kasino ya Mtandaoni

CHEZA SASA

Acha ujumbe