Mambo bado ni magumu kwa Chelsea kunako soko la usajili kueleka msimu ujao. Inter Milan wamewakataa mchana kweupe!
Baada ya kuambulia patupu kwenye harakati za kutaka kumsajili Erling Haaland, The Blues walihamishia majeshi yao kwa Romelu Lukaku, “A Big No” ndio walichokutana nacho.
Mkurugenzi Mkuu wa Inter – Marotta ameweka wazi kuwa klabu hiyo hainampango wa kumuuza mchezaji yeyote tegemezi kwenye kikosi hicho. Tayari Inter wamemuuza Ashraf Hakimi na sasa hawauzi mchezaji mwingine yeyote wa kikosi cha kwanza.
Chelsea wameripotiwa kutoa dau la euro 100M pamoja na Marcus Alonso kama sehemu ya kumsajili Lukaku lakini pendekezo lao limekataliwa mchana kweupe. Lukaku mwenyewe alishasema anafuraha sana kuwepo Inter na hana mpango wowote wa kuondoka klabuni hapo siku za karibuni.
Unakila sababu ya kuwa moja ya mamilionea katika kasino za mtandaoni za meridianbettz, Mchezo wa Ruby Casino Queen unaweza kukufanya ujishindie mkwanja mrefu. Furahia ubora wa kasino zetu na njia kibao za kuwa mshindi leo hii ukiwa na mrembo Ruby.!
Sania+mapua
Pole yao