Klabu ya Chelsea baada ya kujitoa kwenye mbio za kunasa saini ya winga wa klabu ya Cystal Palace Michael Olise sasa wamehamia kwa winga wa klabu ya Athletic Club Nico Williams raia wa kimataifa wa Hispania.
Chelsea walikua wanamuhitaji winga Michael Olise lakini baada wakajitoa kwenye mbio hizo na winga huyo akaamua kujiunga na klabu ya Fc Bayern Munich ya nchini Ujerumani, Inaonekana nguvu zimehamia kwa kijana mdogo Nico W illiams mwenye umri wa miaka (21).Winga Nico Williams amekua kwenye kiwango bora sana ndani ya klabu ya Athletic Club jambo ambalo limefanya vilabu kadhaa kumtolea macho barani ulaya, Mbali na Chelsea lakini pia klabu ya Barcelona wanaelezwa kumuhitaji sana winga huyo mwenye kipaji kikubwa.
Chelsea wanahitaji kukiboresha kikosi chao kuelekea msimu ujao chini ya kocha Enzo Maresca ili kufanya vizuri na kuepuka msimu mbaya ambao wameupata msimu uliomalizika, Hivo jambo kubwa ambalo wanalifanya kwasasa ni kuhakikisha wanaingia sokoni kutafuta wachezaji wenye ubora.Matajiri hao wa jiji la London wanaelezwa kua walikua wanamuhitaji Nico Williams tangu msimu uliomalizika lakini hawakufanikiwa kupata saini yake, Hivo msimu huu wanahitaji kuharakisha dili hilo kwakua wanajua fika wakichelewa wanaweza kumkosa mchezaji huyo kwakua wanaomuhitaji sio wao tu.
This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.
Strictly Necessary Cookies
Strictly Necessary Cookie should be enabled at all times so that we can save your preferences for cookie settings.
If you disable this cookie, we will not be able to save your preferences. This means that every time you visit this website you will need to enable or disable cookies again.