Chelsea Wamepata Majibu Kuhusu Nia Yao ya Kumsajili Beki wa Arsenal, Riccardo Calafiori.

Inaonekana kuwa vigumu kwa Chelsea kukamilisha uhamisho wao walioutaka wa Riccardo Calafiori kutoka kwa wapinzani wao wa London, Arsenal, kwa mujibu wa Caught Offside.

Chelsea Wamepata Majibu Kuhusu Nia Yao ya Kumsajili Beki wa Arsenal, Riccardo Calafiori.

Nia ya Chelsea kwa beki huyo wa Italia iliripotiwa wiki chache zilizopita, huku ikielezwa kuwa timu hiyo imekuwa ikimfuatilia kwa muda mrefu, hata tangu walipotaka kumsajili kabla ya kujiunga na Arsenal.

Ripoti hiyo pia ilieleza kuwa mchezaji huyo anatamani kupata muda zaidi wa kucheza, jambo linaloweza kumfanya afikirie kuondoka Emirates.

Kwa sasa, Calafiori ameanza takriban nusu ya mechi 31 za EPL ambazo Arsenal wamecheza msimu huu, na anaonekana kutaka kuwa chaguo la kwanza sehemu nyingine.

Hata hivyo, Caught Offside wanaripoti kuwa ni vigumu kwa Chelsea kumpata. Sababu kuu ni mbili kwanza, Arsenal hawako tayari kumuuzia mpinzani wao wa moja kwa moja, na pili, Calafiori anapendelea kurejea Italia ambako kuna vilabu vingi vinavyomtaka.

Meridianbet inakwambia kuwa endelea kubashiri hapa kwani ODDS KUBWA na machaguo zaidi ya 1000 yapo hapa. Ingia kwenye akaunti yako na uanze safari yako ya ushindi sasa.

Kabla ya kujiunga na Arsenal, beki huyo aliwahi kucheza katika vilabu vya Italia kama AS Roma, Genoa na Bologna, ambapo aling’ara na kuvutia usajili wake kwenda Uingereza.

Chelsea Wamepata Majibu Kuhusu Nia Yao ya Kumsajili Beki wa Arsenal, Riccardo Calafiori.

Kiwango chake akiwa Arsenal kimevutia Inter Milan, ambao wanamfuatilia kwa karibu. Inaelezwa kuwa Alessandro Bastoni anaweza kuhamia FC Barcelona, na iwapo hilo litatokea, Inter wanataka kumchukua Calafiori kama mbadala wake.

Hata hivyo, Arsenal bado hawako tayari kumpoteza beki huyo wa Italia, na yeye mwenyewe hajaanza kusukuma kuondoka kwa sasa. Lakini Inter wanaona nafasi ya kutumia hali ya kupungua kwa nafasi yake kikosini, hasa baada ya kushuka nyuma ya Piero Hincapié kwenye uchaguzi wa kikosi.

Chanzo kimoja kilisema: “Calafiori hasukumi kuondoka Arsenal kwa sasa, lakini ameanza kupoteza nafasi kikosini msimu huu, hivyo Inter wanaona ni dili linalofaa kuchunguzwa. Anatamani kurudi Italia siku moja, na ingawa inaweza kuwa mapema kuliko ilivyotarajiwa, uwezekano huo hauwezi kupuuzwa majira haya ya joto.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.