Inaonekana kuwa vigumu kwa Chelsea kukamilisha uhamisho wao walioutaka wa Riccardo Calafiori kutoka kwa wapinzani wao wa London, Arsenal, kwa mujibu wa Caught Offside.

Nia ya Chelsea kwa beki huyo wa Italia iliripotiwa wiki chache zilizopita, huku ikielezwa kuwa timu hiyo imekuwa ikimfuatilia kwa muda mrefu, hata tangu walipotaka kumsajili kabla ya kujiunga na Arsenal.
Ripoti hiyo pia ilieleza kuwa mchezaji huyo anatamani kupata muda zaidi wa kucheza, jambo linaloweza kumfanya afikirie kuondoka Emirates.
Kwa sasa, Calafiori ameanza takriban nusu ya mechi 31 za EPL ambazo Arsenal wamecheza msimu huu, na anaonekana kutaka kuwa chaguo la kwanza sehemu nyingine.
Hata hivyo, Caught Offside wanaripoti kuwa ni vigumu kwa Chelsea kumpata. Sababu kuu ni mbili kwanza, Arsenal hawako tayari kumuuzia mpinzani wao wa moja kwa moja, na pili, Calafiori anapendelea kurejea Italia ambako kuna vilabu vingi vinavyomtaka.
Meridianbet inakwambia kuwa endelea kubashiri hapa kwani ODDS KUBWA na machaguo zaidi ya 1000 yapo hapa. Ingia kwenye akaunti yako na uanze safari yako ya ushindi sasa.
Kabla ya kujiunga na Arsenal, beki huyo aliwahi kucheza katika vilabu vya Italia kama AS Roma, Genoa na Bologna, ambapo aling’ara na kuvutia usajili wake kwenda Uingereza.



