Aliyekua mshambuliaji wa timu ya vijana ya Arsenal mwenye kipaji kikubwa Chido Obi Martin (16) amefanikiwa kukamilisha vipimo vyake vya afya ndani ya Man united.
Chido Obi Martin amekua akionesha ubora mkubwa sana ndani ya timu ya vijana ya Arsenal licha ya kua na umri mdogo wa miaka 16 tu, Klabu ya Manchester United ilivutiwa na mchezaji huyo kinda na kumshawishi ajiunge na klabu yao wakimuahidi kumpatia nafasi ya kucheza kwenye timu ya wakubwa.



