Kocha wa timu ya Tottenham spurs Antonio Conte amekubali kua atakuwa na furaha kumuona mchezaji wa timu ya Brentford Christian Eriksen wikiendi hii kwenye mchezo wa kufa na kupona rimu hizo zinapokwenda kukutana.
Conte alimsaini Eriksen akitokea klabu ya Tottenham kipindi anafaundisha klabu ya Inter Milan mwaka 2020, Eriksen alikuwa mtu muhimu kwenye mbio za ubingwa wa Serie A ambao walifanikiwa kuuchukua.
Eriksen kwa sasa anaichezea klabu ya Brentford tokea arejee baada ya kupata matatizo ya moyo kwenye michuano ya ulaya akiwakilisha taifa lake la Denmark.
“Nina furaha kumuoana akicheza tena. Mwezi June ulikuwa mbaya, picha zote mbaya na ilikuwa mbaya kwa kila mtu, Tumeteseka sana kwa ajiri yake na familia yake. Conte alimwambia mwandishi.
“Kumuona machezoni tena itakuwa furaha kubwa kwangu. Ni ajabu kwa kile kilichotea siku nyingi zilizopita.
“Kumuoana akicheza tena kunanifanya niwe na furaha kubwa kwa sababu najua maisha ya mpira, kupata nafasi hii ni jambo kubwa kwake na familia yake kwasababu wanaweza kurudi kwenye maisha yao ya kawaida.”
Maana halisi ya ushindi mkubwa unaipata katika kasino ya mtandaoni ya Aviator kutoka meridianbettz. Andaa kapu la ushindi wa mkwanja na beti kibao za BUREEE.