Cristiano Ronaldo Afikisha Magoli 750!

Ligi ya Mabingwa inaendelea kuweka rekodi mbalimbali katika ulimwengu wa soka. Mchezo wa Juventus vs Dynamo Kiev, umetumika kuweka rekodi ya Cristiano Ronaldo.

Cristiano Ronaldo alipachika goli katika dakika ya 57 kwenye ushindi wa 3-0 na goli hilo licha ya kuwapa ushindi Juve, lakini pia limeweka rekodi kwa mchezaji huyu kufikisha magoli 750 tangu ameanza kucheza soka.

Akiwa ni mshindi mara 5 wa tuzo ya Ballon d’Or, alipokuwa Madrid alifunga magoli 450 katika michezo 438, na wakati akiwa United, alifunga jumla ya magoli 118. Goli la jana dhidi ya Dynamo Kiev, ni goli lake la 75 akiwa na Juventus.

Kwa siku za karibuni, Ronaldo aliweka rekodi nyingine kwa kufikisha zaidi ya magoli 100 akiwa na timu ya Taifa ya Ureno. Idadi hii ya magoli inamfanya Ronaldo awe mchezaji wa 2 duniani nyuma ya Ali Daei wa Iran kama wachezaji wenye magoli mengi katika timu za taifa.

Ronaldo Akishangilia Baada ya kupachika goli dhidi ya Dynamo Kiev

Mpaka sasa, Ronaldo anaendelea kutamba kama mfungaji wa muda wote wa Real Madrid akiwa amemzidi Raul kwa jumla ya magoli 127.

Baada ya kuweka rekodi hiyo, Cristiano Ronaldo aliwashukuru wachezaji wenzake, kocha na wapinzani wake kwa kuwa na mchango katika kufikia hatua hiyo.

Ronaldo alisema ” magoli 750, nyakati za furaha 750, nyuso 750 za furaha kwa mashabiki wetu. Ninawashukuru wachezaji na makocha wote ambao wamenisaidia kuifikia hii namba, ninawashukuru wapinzani wangu wote kwa kunifanya niongeze juhudi katika utendaji kazi wangu.”

Mchezo wa Juventus dhidi ya Torino wikiendi hii utakuwa ni safari nyingine ya Ronaldo kulitafuta goli la 751. Katika mechi 4 dhidi ya Torino, Ronaldo amefunga kwenye mechi 3.


FURAHIA MUZIKI MTANDAONI HUKU UKITENGEZA MKWANJA!!

Mchezo wa Astro Legend unakupatia burudani ya muziki kupitia kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!

INGIA MCHEZONI

26 Komentara

    CR7 hana mpinzani

    Jibu

    Pongezi nyingi kwake

    Jibu

    Anastahili pongezi 👏👏

    Jibu

    Cr7 noma sana

    Jibu

    Aaaah hongera yake ronaldo huyo Mimi ninamuita mlipiza visasa wa magoli huwa kama amepoteza kufunga goli ujue wakati mwingine itamlazimu apate goli ili atomize lengo lake la kucheka na nyavu

    Jibu

    Hongera sana Ronaldo

    Jibu

    Safii Sana Ronaldo

    Jibu

    CR7 ni moto wa kuotea mbali

    Jibu

    CR7 he is the best

    Jibu

    Cr7 yupo vizuri

    Jibu

    Huyo ndo Cr7 bwana moto wa kuotea mbali

    Jibu

    Ronaldo ataweza kuvunja rekodi ya Pele?

    Jibu

    Duh Ronaldo yupo vizur

    Jibu

    Cr7 n habar nyingine

    Jibu

    Congrats Cr7 mwamba wa kuvunja record za malegend wa soka

    Jibu

    Aaaah hongera yake ronaldo huyo Mimi ninamuita mlipiza visasa wa magoli huwa kama amepoteza kufunga goli ujue wakati mwingine itamlazimu apate goli ili atomize lengo lake la kucheka na nyavu

    Jibu

    Mmh cr 7 rekod za kibabe

    Jibu

    Nice one

    Jibu

    Katisha kinyama

    Jibu

    Pongz kwake

    Jibu

    Cr7 MTU mbaya

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Mnyama Cr7

    Jibu

    Madogo sana

    Jibu

Acha ujumbe