Ligi ya Mabingwa inaendelea kuweka rekodi mbalimbali katika ulimwengu wa soka. Mchezo wa Juventus vs Dynamo Kiev, umetumika kuweka rekodi ya Cristiano Ronaldo.
Cristiano Ronaldo alipachika goli katika dakika ya 57 kwenye ushindi wa 3-0 na goli hilo licha ya kuwapa ushindi Juve, lakini pia limeweka rekodi kwa mchezaji huyu kufikisha magoli 750 tangu ameanza kucheza soka.
Akiwa ni mshindi mara 5 wa tuzo ya Ballon d’Or, alipokuwa Madrid alifunga magoli 450 katika michezo 438, na wakati akiwa United, alifunga jumla ya magoli 118. Goli la jana dhidi ya Dynamo Kiev, ni goli lake la 75 akiwa na Juventus.
Kwa siku za karibuni, Ronaldo aliweka rekodi nyingine kwa kufikisha zaidi ya magoli 100 akiwa na timu ya Taifa ya Ureno. Idadi hii ya magoli inamfanya Ronaldo awe mchezaji wa 2 duniani nyuma ya Ali Daei wa Iran kama wachezaji wenye magoli mengi katika timu za taifa.

Mpaka sasa, Ronaldo anaendelea kutamba kama mfungaji wa muda wote wa Real Madrid akiwa amemzidi Raul kwa jumla ya magoli 127.
Baada ya kuweka rekodi hiyo, Cristiano Ronaldo aliwashukuru wachezaji wenzake, kocha na wapinzani wake kwa kuwa na mchango katika kufikia hatua hiyo.
Ronaldo alisema ” magoli 750, nyakati za furaha 750, nyuso 750 za furaha kwa mashabiki wetu. Ninawashukuru wachezaji na makocha wote ambao wamenisaidia kuifikia hii namba, ninawashukuru wapinzani wangu wote kwa kunifanya niongeze juhudi katika utendaji kazi wangu.”
Mchezo wa Juventus dhidi ya Torino wikiendi hii utakuwa ni safari nyingine ya Ronaldo kulitafuta goli la 751. Katika mechi 4 dhidi ya Torino, Ronaldo amefunga kwenye mechi 3.
Mchezo wa Astro Legend unakupatia burudani ya muziki kupitia kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!




Sabrina
CR7 hana mpinzani
Magdalena
Pongezi nyingi kwake
Adelta
Anastahili pongezi 👏👏
Khadija
Cr7 noma sana
Fatina mfingi
Hii hatar sasa
Ester jackson
Aaaah hongera yake ronaldo huyo Mimi ninamuita mlipiza visasa wa magoli huwa kama amepoteza kufunga goli ujue wakati mwingine itamlazimu apate goli ili atomize lengo lake la kucheka na nyavu
Caroline
Hongera sana Ronaldo
Lydia Emmanuel Magoti
Safii Sana Ronaldo
Ernest
CR7 ni moto wa kuotea mbali
Samira
CR7 he is the best
Tatu
Cr7 yupo vizuri
Dorophina
Huyo ndo Cr7 bwana moto wa kuotea mbali
Sylvester
Ronaldo ataweza kuvunja rekodi ya Pele?
Fatuma kasomo
Duh Ronaldo yupo vizur
Asia Abdy
Cr7 n habar nyingine
Povel
Congrats Cr7 mwamba wa kuvunja record za malegend wa soka
David Pere
Aaaah hongera yake ronaldo huyo Mimi ninamuita mlipiza visasa wa magoli huwa kama amepoteza kufunga goli ujue wakati mwingine itamlazimu apate goli ili atomize lengo lake la kucheka na nyavu
Issa
Mmh cr 7 rekod za kibabe
Latifa juma mohamed
Nice one
Hopemwaikuka
Katisha kinyama
Janeflora malisa
Pongz kwake
[email protected]
Mnyama cr 7
Saupha mohamed
Cr7 MTU mbaya
Mariam mtandama
Safi
samiah
Mnyama Cr7
warda
Madogo sana