Cristiano Ronaldo Akanusha Taarifa za Kujiunga na Al Nassr

Cristiano Ronaldo amevunja ukimya wake kuhusu ripoti zinazomhusisha na kuhamia klabu ya Al Nassr ya Saudi Arabia akisisitiza kuwa ‘sio kweli’.

 

ronaldo

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 37 aliondoka Manchester United mwezi uliopita baada ya uhusiano wake kuvunjika na wakuu wa klabu kuwa mbaya zaidi alipotoa kauli nyingi za kutatanisha katika mahojiano ya televisheni na Piers Morgan.

Tangu kuondoka kwake Old Trafford, uvumi umeenea kuhusu klabu gani Ronaldo atajiunga, huku mshambuliaji huyo akiwa mchezaji huru kuelekea nusu ya pili ya msimu.

Ripoti ziliibuka Jumatatu ambazo zilidokeza kwamba nyota huyo ambaye amemaliza mkataba wake yuko mbioni kukubaliana na Al Nassr mkataba mkubwa ambao ungemfanya mshindi huyo mara tano wa tuzo ya Ballon d’Or apate kiasi cha Euro milioni 200 (£173m) kwa msimu.

 

ronaldo

Chombo cha Hispania MARCA kiliripoti kwamba Ronaldo, ambaye kwa sasa ni mchezaji huru alikuwa tayari kusaini mkataba na klabu ya Mashariki ya Kati mwanzoni mwa mwezi ujao.

Kampuni hiyo ilidai kuwa mkataba wa awali ulikuwa na thamani ya karibu €100m (£86m) lakini ungechochewa na makubaliano zaidi kama vile matangazo na mikataba ya udhamini.

Hata hivyo, kufuatia ushindi wa Ureno wa mabao 6-1 dhidi ya Uswizi katika hatua ya 16 bora ya Kombe la Dunia, ambapo Ronaldo alianzia benchi na nafasi yake kuchukuliwa nashujaa wa hat-trick, Goncalo Ramos, supastaa huyo mkongwe alikanusha tetesi zinazomhusisha na kuhamia Mashariki ya Kati.

“Hapana, hiyo si kweli – si kweli,” aliwaambia waandishi wa habari baada ya mchezo huo.

Pendekezo la Al Nassr liliripotiwa kuwa la miaka miwili na nusu hadi msimu wa joto wa 2025.

Vyanzo vilivyo karibu na Ronaldo siku ya Jumatatu vilibainisha kuwa ripoti za kukamilika kwa mkataba huo ni ‘upuuzi’.

Fowadi huyo hapo awali hakuwa ametoa maoni yoyote kuhusu mustakabali wake,  wakati wa kampeni za Kombe la Dunia lakini sasa inaonekana kana kwamba hatahamia Saudi Arabia.

Katika mahojiano yaliyotajwa hapo juu na Morgan, Ronaldo alikiri tetesi za ofa ya Euro milioni 350 kwa misimu miwili kutoka kwa klabu ya Saudi Arabia ambayo haikutajwa jina msimu wa joto ni kweli jambo ambalo alilikataa.

Al-Nassr ni moja ya vilabu vilivyofanikiwa zaidi nchini Saudi Arabia, ikiwa imetawazwa washindi wa ligi kuu ya nchi hiyo mara tisa, na ushindi wao wa hivi karibuni ni mnamo 2019.

Beti mechi zijazo za kombe la dunia na nyingine kupitia Meridianbet, beti na kitochi bila bando, kwenye machaguo spesho ya kombe la dunia yenye ODDS kubwa na bomba, na kama sio mpenzi wa mpira kuna michezo ya kasino mtandaoni napo unaweza kushinda jakipoti kubwa. Beti hapa.

Acha ujumbe