Beki wa kushoto wa klabu ya Chelsea Marc Cucurella ameweka wazi kua wana furaha kubwa kama wachezaji kutokana na uteuzi wa kocha mpya wa klabu hiyo Enzo Maresca.
Cucurella amesema kocha huyo amefanya kazi nzuri ndani ya klabu ya Leicester City hivo wamempokea kwa mikono miwili kocha huyo kuelekea msimu ujao ndani ya klabu ya Chelsea akianza majukumu yake ndani ya klabu ya klabu hiyo matajiri wa jiji la London.
Kocha Enzo Maresca amejiunga na klabu ya Chelsea kuchukua mikoba ya aliyekua kocha wa klabu hiyo msimu uliomalizika Mauricio Pochettino, Anakuja ndani ya klabu hiyo kwajili ya kuhakikisha anairudisha timu hiyo kwenye mstari baada ya mfupa huo kuwashinda makocha takribani wanne sasa.
Kocha Maresca amekua na ubora mkubwa sana ndani ya klabu ya Leicester City ambayo ameirudisha ligi kuu ya Uingereza, Jambo ambalo limewapa imani kubwa mabosi wa Chelsea wakiamini kocha huyo ni mtu sahihi wa kuirudisha klabu hiyo kwenye ubora wake.Kama ambavyo Cucurella ameonesha upendo na kumpokea kocha huyo kuelekea msimu ujao vivo hivyo wachezaji wengine wanatarajiwa kumpokea kocha huyo, Kwani tayari ndio mwalimu mpya wa klabu hiyo na wanapaswa kumpa ushirikiano ili kuweza kufanya kazi vizuri.
This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.
Strictly Necessary Cookies
Strictly Necessary Cookie should be enabled at all times so that we can save your preferences for cookie settings.
If you disable this cookie, we will not be able to save your preferences. This means that every time you visit this website you will need to enable or disable cookies again.