Dayot Upamecano - Lulu Inayowindwa na Wengi.

Beki wa RB Leipzig na timu ya Taifa ya Ufaransa – Dayot Upamecano anaendelea kuviteka vichwa vya habari ulimwenguni kuhusu hatma yake kwenye ulimwengu wa soka.

Ni nani ataipata lulu hii ambayo inaonekana kama ndio tiba ya timu nyingi barani Ulaya zinazotaabika kwenye safu zao za ulinzi?

Akiwa na umri wa miaka 22 pekee, Dayot Upamecano anahusishwa kujiunga na vilabu mbalimbali. Liverpool, Manchester United, Bayern Munich na Real Madrid ni miongoni mwa timu zinazoiwinda saini ya beki huyu mahiri.

Mkataba wa Upamecano ndani ya Leipzig unakipengele cha kuruhusu mchezaji huyo kuuzwa kwa dau la pauni milioni 40 mwishoni mwa msimu huu. Japokuwa, taarifa zimeripoti uwezekano wa beki huyo kuuzwa mapema mwezi Januari kama tu, timu itafikia dau lililopo kwenye mkataba wake.

Inasemekana Bayern Munich wamejitoa kwenye mbio za kuisaka saini ya Dayot Upamecano kutokana na sababu za kiuchumi. Licha ya kwamba Bayern huenda ikawakosa mabeki wake wawili – David Alaba na Jerome Boateng mwishoni mwa msimu kufuatia kuisha kwa mikataba yao, bado dau la Upamecano ni kubwa kwa Bayern kujitosa sokoni.

Kwa upande wa Madrid, inaaminika kocha – Zinedine Zidane anamtizama Upamecano kama mrithi sahihi wa nahodha wa kikosi hicho – Sergio Ramos. Ikiwa mpaka sasa hatma ya Ramos haijajulikana, huenda Madrid wakajitosa kuingia sokoni mapema na kuitafuta saini ya Upamecano.

Nchini uingereza kuna vita ya aina yake linapokuja suala la usajili. Liverpool na Manchester United ni mahasimu wa Ligi Soka nchini Uingereza. Kwa miaka mingi wamekuwa hawauziani wachezaji kutokana na uhasimu wao. Hapa takayempata Upamecano atakuwa ameshinda vita kubwa.

Liverpool inataabika na idadi kubwa ya majeruhi kwenye kikosi hicho. Mpaka sasa, wachezaji wote wa safu ya ulinzi wanaocheza kikosi cha kwanza ni majeruhi na watakuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu. Hili ni pigo kwa Jurgen Klopp na atalazimika kuingia sokoni mapema iwezekanavyo.

Je, Klopp atajitosa kumsajili Dayot Upamecano kwa dau lililowekwa au wataamua kuwatumia wachezaji wao wenye uwezo wa kuziba mapengo kwenye safu ya ulinzi? Hili bado ni swali ambalo majibu yake pengine yatapatikana kuanzia Januari 1, 2021.

Ole Gunnar Solskjaer bado hajatibu tatizo kwenye safu yake ya ulinzi licha ya kuwasajili Aaron Wan-Bissaka, Harry Maguire na Alex Telles kama walinzi wa miamba hiyo ya Old Trafford.

United wanahitaji beki wa kati mwenye kasi ya kuanzisha na kuzuia mashambulizi na atakayeweza kucheza vizuri na Harry Maguire ambaye hana kasi kubwa katika uchezaji wake. Dayot Upamecano alitajwa sana kama mchezaji anayehitajika zaidi kwenye kikosi cha United lakini usajili wake haukuwezekana katika dirisha la usajili lililopita. Je, Januari United wataweka pesa mezani na kumchukua mchezaji wanayemuwinda kwa muda mrefu?

Uwezo wake wa kuanzisha mashambulizi na kulinda timu yake pamoja na kufunga magoli, ni kati ya vitu vikubwa alivyonavyo Upamecano. Umri wake ni mdogo na hivyo ni faida kwa timu yeyote itakofanikiwa kuipata huduma yake.


BASHIRI UKIWA MAHALI POPOTE!

Hauhitaji kuwaza linapokuja suala la ubashiri na odds kubwa. Bashiri na Meridianbet ukiwa popote ufurahie ushindi mkubwa katika michezo mbalimbali na hadi milioni 16 kwenye michezo ya kasino.

Meridianbet Beti Popote

INGIA MCHEZONI!

24 Komentara

    Goodupdate

    Jibu

    Upamecano ana rekodi nzuri sana

    Jibu

    Yupo vizuri

    Jibu

    Safii sana

    Jibu

    Rekodi yake nzuri ndio inapelekea kuwindwa na wengi na yoyote atakaefanikiwa kumpata anatakua msaada mkubwa hasa kwa timu ambazo bado hazifanyi vizuri

    Jibu

    Dayot Upamecano alicheza vizuri mno mechi ya LEIPZIG dhidi ya PSG hilo lilimuweka kwenye rada za Klabu duniani

    Jibu

    Dayot yupo vizuri

    Jibu

    Bora aende real Madrid akawike vizuri

    Jibu

    Dayot nimemuelewa

    Jibu

    Nice

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Good

    Jibu

    Yupo vizur

    Jibu

    Anajua ndio maana wanamgombea

    Jibu

    Dayot anajua

    Jibu

    yupo vizuriii

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Inasemekana Bayern Munich wamejitoa kwenye mbio za kuisaka saini ya Dayot Upamecano kutokana na sababu za kiuchumi. Licha ya kwamba Bayern huenda ikawakosa mabeki wake wawili – David Alaba na Jerome Boateng mwishoni mwa msimu kufuatia kuisha kwa mikataba yao, bado dau la Upamecano ni

    Jibu

    Upamecano lulu iatakasumbua kwenye soka

    Jibu

    kijana yupo vizuri ndo maana analiliwa na wengi

    Jibu

    Ni wakati wake sasa Dayot Upamecano kulamba deal nono

    Jibu

    Subili tuangalie mtazamo wake mwenyew clabu hipi hataenda kuichezea

    Jibu

    Dodo limekwiva kaz kwao walaj

    Jibu

    Nice update

    Jibu

Acha ujumbe