Kocha wa Spain, Luis de la Fuente, ametoa kauli kali dhidi ya wachezaji wa Argentina kufuatia vurugu zilizotokea baada ya fainali ya Kombe la Dunia 2026. Hispania walitwaa ubingwa kwa mara ya pili katika historia yao kwa ushindi wa 1-0 baada ya muda wa nyongeza dhidi ya Argentina kwenye MetLife Stadium, lakini sherehe ziligeuka vurugu.

De la Fuente alisema kupitia televisheni ya Hispania, “Kilichotokea baada ya mechi hakiwezi kukubalika kwa hali yoyote. Tulichokiona hakivumiliki na hakikubaliki. Wachezaji wa kiwango hiki, wakiongozwa na kocha mkubwa, lazima walihisi vibaya walipoona matukio hayo. Hizi ni taswira zisizostahili soka.”
Baada ya mchezo huo wa fainali, vurugu ziliibuka pale Leandro Paredes alipotumia nguvu na kufanya makabiliano ya moja kwa moja na wachezaji wa Hispania hasa hasa Gavi na Eric Garcia. Nahuel Molina alimpiga Rodri. Vilevile, Fabian Ayala, msaidizi wa Lionel Scaloni, anatuhumiwa kumshambulia Dani Olmo.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kocha wa La Roja aliwasifu wachezaji wake kwa kutulia na kuonyesha ustaarabu licha ya uchokozi huo. “Ningependa kupongeza tabia ya wachezaji wetu kwa namna walivyodhibiti hali na kuonyesha sportsmanship hadi mwisho,” alisema.

FIFA imefungua uchunguzi rasmi ili kubaini wahusika na kutoa adhabu stahiki. Tukio hili limeibua mjadala mkubwa kuhusu nidhamu na heshima katika soka la kimataifa, hasa kwa wachezaji wa kiwango cha juu.



