Mchezaji namba moja kwa ubora Duniani kwa mchezo wa Tennis Novak Djokovic, ameingia nusu fainali ya Grand Slam ya kwanza ya msimu wa mwaka 2021 (Australian Open) .
Baada ya upinzani mkali kutoka kwa kijana wa Kijerumani Alexander Zverev ambaye anashika namba 7 ya ubora duniani, ilimchukua mwamba huyo wa Serbia masaa 3 :29 kushinda kwa seti 3-1 ambapo alipoteza seti ya kwanza kwa tie-break (7, 6) na kushinda (6,4 6,2 7,6).
Sasa Djokovic anakutana na Aslan Karatsev ambaye anashika nafasi ya 114 katika ubora huko yeye akiwa namba 1. Karatsev ameingia nusu baada ya kumtwanga majeruhi Grigor Dimitrov kwa seti 3-1.
Mrusi huyo ameingia kwenye rekodi kuwa mchezaji wa 5 ambaye alipitia kwenye mchujo na baadae kufika nusu fainali. Huku Djokovic akifikia nusu fainali yake ya 9 ya Australian Open.
Treasure Heroes inakupa nafasi ya kupambania ushindi wako mkubwa kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet! Usisubiri hii, jiunge sasa kufurahia ushindi!
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri
neema hassan
Habar njema kwa mashabik
Sadick
Hongera kwake.anarudi kwenye kiwango chake. Kuna uwezekano akashinda.
warda
Hongera yake
Rahma
Safiii
Caroline
Hongera sana Djokovic
Sarah
Safii
Angelina
Nice
Dorophina
Pongezi kwake
Hopemwaikuka
Congrats